Skip to main content

Mwalimu mashakani kwenda jela Marekani kwa kumnyoa mwanafunzi nywele kwa lazima

Margaret Gieszinger alikamatwa baada ya video ya kisa hicho kusambazwa mtandaoni                                                               Margaret Gieszinger

Mwalimu mmoja nchini Marekani anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu, baada ya picha ya video kusambaa mitandaoni akimkata kwa lazima nywele mwanafunzi mmoja darasani, huku akiimba wimbo wa taifa wa Marekani.
Margaret Gieszinger, 52, amefukuzwa kazi kwa kitendo hicho alichokifanya katika Shule ya Sekondari ya Chuo Kikuu cha huko Visalia, California.
Waendesha mashtaka wamesema kuwa amekanusha makosa sita dhidi yake, likiwemo kosa la ukatili dhidi ya mtoto na shambulio la kimwili. Anakabiliwa na hukumu ya miaka mitatu unusu jela iwapo atakutwa na hatia.

Bi Gieszinger, aliachiliwa kwa dhamana ya dola 100,000 Ijumaa jioni.
Katika video hiyo ya iliyochukuliwa kwa simu ya mkononi kisha kupakiwa kwenye mtandao wa Reddit, mwalimu huyo anayefunza somo la sayansi, anaonekana akimuita mwanafunzi wa kiume kuketi mbele ya darasa, kisha akaanza kumkatakata nywele huku akiimba kwa makosa wimbo wa taifa la Marekani maarufu kama Star Spangled Banner.
Wakili wa mwanafunzi huyo, ameliambia shirika la habari la CNN kuwa, mteja wake "alishtuka sana" kabla ya kufanikiwa kujinasua mikononi mwa mwalimu huyo.
Bi Gieszinger kisha anaonekana kwenye video, akishika mkasi mkononi juu ya kichwa chake na kusema "next!" yaani "mwingine!" na kutishia pia kumkata nywele mwanafunzi mmoja wa kike.
"Tunachukulia kwa tahadhari kubwa mno usalama wa wanafunzi madarasani," hiyo ni kwa mjibu wa taarifa kutoka kwa afisi kuu ya Elimu ya kaunti ya Tulare.
"Tunachunguza taarifa zote tunazozipokea na tutachukua hatua kali mno na zinazohitajika dhidi ya wafanyakazi wetu walio na utovu wa nidhamu." Taarifa hiyo imeongeza.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...