Skip to main content

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Rayvanny
Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).
Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono."
Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile.
"Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza.
Ujumbe wa Twitter wa @BasataTanzania: Wimbo wa Msanii Ray Vanny wa #Mwanza aliomshirikisha msanii Diamond umefungiwa rasmi kwa kubeba maudhui machafu. Lebo ya Wasafi, wasanii wake sambamba na vyombo vya habari vinapewa onyo na tahadhari kuendelea kutumia wimbo huu kwa namna yoyote ile. #SanaaKazi #Maadili

Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa zote ambazo walisambaza.
Basata wamekuwa mstari wa mbele nchini Tanzania kufungia nyimbo ambazo wamekuwa wakidai zinaenda kinyume na maadili. Katika miaka ya hivi karibuni, nyimbo ambazo zimeonekana zikiukosoa utawala wa Rais John Magufuli pia zimekuwa zikichukuliwa hatua kali nchini Tanzania.
Mwezi Juni mwaka huu, Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi, maarufu kwa jina la Sugu alitangaza mpango wake wa kulishtaki baraza hilo baada ya kuufungia wimbo wake.
Basata ilitangaza kufungiwa kwa wimbo mpya wa Sugu unaoitwa 219 kwa madai kuwa una ujumbe wenye uchochezi. Mpaka sasa bado Sugu hajawasilisha suala hilo mahakamani.
Diamond si mgeni wa kufungiwa nyimbo zake na Basata, mwezi Februari vibao v
yake viwili Hallelujah (uliomshirikisha Morgan Heritage ) na Waka Waka (uliomshirikisha Rick Ross) vilifungiwa.
Wakati huo Diamond alikuwa katika fungu moja na wasanii wengine 10 ambao walichukuliwa hatua hizo na Basata.

Nyimbo mbili za Ney wa Mitego, jina lake halisi Emmanuel Elibariki - Pale kati Patamu na Maku Makuz - pia zimefungiwa.
Mwanamuziki Roma Mkatoliki ambaye jina lake halisi ni Abernego Damiani naye amefungiwa wimbo wa Kibamia.
Wimbo wa Amani Hamisi maarufu kama Manifango wa Hainaga Ushemeji pia umefungiwa, sawa na I am Sorry JK wake Nikki Mbishi ambaye jina lake halisi ni Nicas John Mchuche.
Nyimbo nyingine ni Tema mate tumchape (Hamad Ali maarufu Madee), Uzuri Wako (Juma Mussa Mpolopoto maarufu Jux), Nampa Papa (Gift Stanford maarufu Gigy Money) na Nampaga (Barnaba Elias maarufu Barnaba).

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...