Skip to main content

Posts

Showing posts with the label MAAJABU

Karl Lagerfeld: Mbunifu wa mitindo amrithisha paka wake Choupette sehemu ya utajiri wake wa mamilioni ya dol

Taarifa zimeibuka kwamba mbunifu mavazi aliyeaga dunia Karl Lagerfeld amemuachia paka wake sehemu ya utajiri wake wenye thamani ya $ milioni 200. Mbunifu huyo, raia wa Ujerumani, ambaye alikuwa mbunifu mkurugenzi wa kampuni za Chanel na Fendi, alifariki Paris Jumanne. Alimlea paka wake wa dhati na alivutia ufahari aliokuwa nao kwa paka wake Choupette tangu alipokabidhiwa mnamo 2012. Lagerfeld ameliambia jarida la Ufaransa Numero mwaka jana  kwamba amemueka paka huyo kwenye wasia wake kama mmoja wa warithi wa makaazi yake ya kifahari. Katika mahojiano hayo, alisema Choupette yumo ndani ya urathi, 'miongoni mwa wengine'. Lakini ameongeza : "Usijali kuna mali ya kumtosha kila mtu." Haki miliki ya pich GES Image caption Lagerfeld akiwa karibu na mchoro wa Choupette Tayari Choupette ana utajiri wa kiasi, akiwa amejipatia $ milioni 3 kutokana na matangazo ya biashara kwa kampuni ya magari Ujerumani na kampuni ya vipodozi ya Japan akiwa na mmiliki wake Lagerfeld. ...

Jinsi mmea uliopandwa na wanaanga wa China ulivyoota mwezini na kukauka

Haki miliki ya picha AFP/CHONGQING UNIVERSITY Mmea uliopandwa na wanaanga wa China mwezini umechukua takriban siku nane kuota. Chombo cha angani Cha china kwa jina Change4 kiliwacha kunyunyuzia maji mbegu hiyo ya pamba kama ilivyopangwa nna Chuo kikuu cha Chongqing ambacho kilitunga jaribio hilo. China ilipata mmea wa kwanza mwezini na kwa nini ni muhimu kuendelea na uchunguzi angani Mmea huo uliota katika chombo ndani ya Change4 ambacho kilitua katika eneo la mbali la ,mwezini mnamo tarehe 3 Januari. Eneo ambalo mmea huo ulikulia usingeweza kuishi katika usiku wa mchana wa Lunar Eclipse. Haki miliki ya picha CNSA Wakati huo wote Ujumbe wote wa China utalazimika kulala na mifumo yao yote italala ili kuhifadhi kawi. Hivyobasi mmea huo haukunyunyuziwa maji na kulazimika kufa , kama ilivyokuwa imepangwa. Majaribio mengine Chombo hicho cha China pia kilibeba mbegu za viazi na arabidopsis, mmea kutoka kwa jamii ya haradali pamoja na matunda na na mayai ya chuchu. Ilitaraj...

Samaki wa Mexico walio na uwezo wa kurekebisha matatizo ya moyo

Haki miliki ya picha BHF Image caption Samaki wa tetra anayeishi katika mito kaskazini mwa Mexico wanaweza kuponya mioyo yao Samaki anayeweza kuurekebisha moyo wake huenda ndio suluhu ya matibabu kwa watu wenye matatizo ya moyo, kwa mujibu wa utafiti. Wanasayansi wanao wachunguza samaki wa Tetra kutoka nchini Mexico wamegundua maeneo matatu ya mfumo wa samaki huyo uliochangia uwezo wake kuunda upya tishu za ndani ya moyo. Jeni moja imeonekana kuwa na jukumu kuu katika mfumo huo. Watafiti wanatumai  utafiti  wao siku moja utafanikisha uponyaji wa misuli ya ndani ya moyo kwa wagonjwa ambao wamewahi kupata mshtuko wa moyo. Maelfu ya watu huishi na matatizo ya moyo baada ya kupata mshtuko wa moyo. Kwasababu binaadamu hawawezi kuunda upya msuli ulioharibika, au kujeruhiwa kwa moyo, na mara nyingi watu hulazimika kuishi na hali hiyo au kuishia kufanyiwa upandikizaji wa moyo. Dalili za samaki kwenye pango Kwa utaifiti huu, uliofadhiliwa na taasisi ya British Heart Foun...

Dermophis donaldtrumpi: Kiumbe anayeishi baharini na nchi kavu apewa jina Donald Trump

  EnviroBuild, ndio kampuni iliyopata haki ya kumpa kiumbe huyo jina, iliongeza nywele bandia kwenye kiumbe huyo jambo lililomfanya kuwa na muonekano unaokaribiana na wa Trump. Kiumbe anayeweza kuishi baharini na katika nchi kavu amepewa jina la Rais wa Marekani Donald Trump, ingawa huenda kiongozi huyo asitake kuhusishwa na kiumbe huyo kutokana na sifa zake. Amfibia huyo huwa anafukia na kuficha kichwa chake mchangani anapokabiliwa na hatari, jambo ambalo pengine limewashawishi wahusika kumpa kiumbe huyo jina la Trump kutokana na kiongozi huyo kukana kwamba shughuli za viwanda na za kibinadamu zinachangia mabadiliko ya tabia nchi. Kiumbe huyo pia ni kipofu, hawezi kuona. Mnyama huyo ambaye amepewa jina Dermophis donaldtrumpi , aligunduliwa katika eneo la Panama, na alipewa jina hilo na mkuu wa kampuni ya EnviroBuild ambaye alikuwa amelipa $25,000 (£19,800) kwenye mnada kupata fursa ya kumpa jina kiumbe huyo. K...

Jengo la kutengenezea ndege aina ya Boeing ndiyo kiwanda kikubwa zaidi duniani

Haki miliki ya picha GETTY IMAGES Image caption Kiwanda hicho sasa kinaunda kizazi kipya cha ndege aina ya Boeing Shirika la Boeing lilipoamua kuunda ndege yake chapa 747 - lilijizolea sifa kwa kufungua mlango wa kutengeneza ndege kubwa zaidi duniani. Hata hivyo shirika hilo lililazimika kujenga kiwanda kikubwa zaidi ambacho kina uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndege hiyo. Ikiwa umewahi kuona ndege aina ya 747 ikiwa karibu, bila shaka utafahamu ukubwa wa ndege hiyo. Kwa hivyo si ajabu kuona kiwanda kilichounda ndege hiyo kuishia kuwa na jumba kubwa zaidi la kiwanda. Jengo  kubwa kiasi gani? Boeing ilianza kujenga kiwanda cha Everett mwaka 1967, muda mfupi baada ya mradi wake wa Boeing 747 kuanza kushika kasi. Bill Allen, mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu katika kampuni ya Boeing, anasema shirika hilo lilifahamu fika kuwa, linahitaji sehemu kubwa, endapo lina mpango wa kuunda ndege ya kubeba abiria 400. Waliamua kuchagua eneo la takriban kilomita 35 Kaskazini mwa jiji la...

Faida tano za kimwili ambazo watu wachache wanazo

Haki miliki ya picha ISTOCK Image caption Kuna watu ambao wana vina saba ambavyo vinawafanya waweze kufanya vitu ambavyo watu wengine hawawezi. Watu hao ambao wana uwezo wa ajabu wa kusadikika kama kwenye katuni na sayansi ya uongo. Lakini baadhi ya binadamu wa kawaida tu huwa wana uwezo wa kipekee jambo ambalo kwa wengine ni ndoto tu kuwa na uwezo kama huo. Katika baadhi ya kesi, huwa wanawakilisha vina saba ambavyo vilifanyiwa mabadiliko na kwa namna nyingine miili yao huwa inaonyesha inavyokubali aina fulani ya maisha. Hii hapa ni mifano ya namna wanavyoweza wa kufanya mambo ambayo wengine hawawezi kufanya. 1.Kuwa na uwezo wa kuona vizuri ndani ya maji Watu wengi hawawezi kuona vizuri wakiwa ndani ya maji. Lakini watoto wa jamii ya Mokeni kutoka makabila matatu ya wanaishi pembezoni mwa pwani ya Myanmar na Thailand wanaweza kuona vizuri jambo ambalo si la kawaida. Watu hawa wa kisiwani wanajulikana kama watu ambao wanahamahama na hutumia muda mwingi kuishi katika vi...