Skip to main content

Jengo la kutengenezea ndege aina ya Boeing ndiyo kiwanda kikubwa zaidi duniani

Kiwanda hicho sasa kinaunda kizazi kipya cha ndege aina ya BoeingHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKiwanda hicho sasa kinaunda kizazi kipya cha ndege aina ya Boeing
Shirika la Boeing lilipoamua kuunda ndege yake chapa 747 - lilijizolea sifa kwa kufungua mlango wa kutengeneza ndege kubwa zaidi duniani.
Hata hivyo shirika hilo lililazimika kujenga kiwanda kikubwa zaidi ambacho kina uwezo wa kukidhi mahitaji ya ndege hiyo.
Ikiwa umewahi kuona ndege aina ya 747 ikiwa karibu, bila shaka utafahamu ukubwa wa ndege hiyo.
Kwa hivyo si ajabu kuona kiwanda kilichounda ndege hiyo kuishia kuwa na jumba kubwa zaidi la kiwanda.
Jengo kubwa kiasi gani?
Boeing ilianza kujenga kiwanda cha Everett mwaka 1967, muda mfupi baada ya mradi wake wa Boeing 747 kuanza kushika kasi.
Bill Allen, mmoja wa viongozi wa ngazi ya juu katika kampuni ya Boeing, anasema shirika hilo lilifahamu fika kuwa, linahitaji sehemu kubwa, endapo lina mpango wa kuunda ndege ya kubeba abiria 400.
Waliamua kuchagua eneo la takriban kilomita 35 Kaskazini mwa jiji la Seattle, karibu na uwanja wa ndege ambao ulitumika kama kituo cha vita wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia.
Ripoti katika jarida la Daily Herald liliangazia eneo hilo lililokuwa tu na barabara ndogo mno ya kufikia barabara kuu ya lami, na hakukuwa na njia ya reli kabisa kuunganisha eneo hilo, huku ukizungukwa na msitu ambao ulikuwa makao ya dubu, waliokuwa wakirandaranda humo.
Boeing ililazimika kujenga kiwanda kipya wakati ilipokuwa ikitengeneza muundo wa ndege ya aina ya 747Haki miliki ya pichaBOEING
Image captionBoeing ililazimika kujenga kiwanda kipya wakati ilipokuwa ikitengeneza muundo wa ndege ya aina ya 747
Wakakati huo huo, Boeing ilikuwa ikijenga mojawepo ya uwanja mkubwa zaidi wa ndege duniani, pia kujenga kiwanda kikubwa zaidi cha kuunda ndege, kuwemo uwanjani humo.
Leo, Kiwanda cha Everett kinapiku jumba lolote lile duniani kwa ukubwa na upana, huku kitabu cha kuandika maswala ya maajabu ya dunia- The Guenness Book of Records, kikiripoti kuwa jumba hilo lina ukuwa wa mita za upana milioni13.3 sawa na futi milioni 472.
"Tulijenga jumba hilo kubwa juu ya baadhi ya maeneo maarufu sana duniani," anasema David Reese, ambaye alikuwa akisimamia usafiri wote wa utalii wa kampuni ya Everett. "Tuko na maeneo maarufu kama vile Versailles, Vatican na Disneyland, na unayaona mara tu unapoanza ziara ya kuzuru kiwanda chetu.
Jumba kuu la Everett, linakaa juu ya ekari 97.8 ya ardhi, mara ukubwa mra 30 zaidi ya viwanja maarufu vya Trafalgar Jijini London.
"Nakumbuka nikifanya mahojiano na BBC miaka michache iliyopita, na nikajiuliza, 'hivi uwanja wa Wembley unaukubwa kiasi gani? Naam, jawabu lake ni kuwa uwanja huo unaingia mara 13 ndani ya eneo lote la kiwanda chetu."
Hadi sasa kampuni ya Everett ingali ikiunda ndege chache za aina ya 747, lakini kwa sasa imejiwekeza zaidi kwenye uundwaji wa aina ndogo za 767, 777 na 787. Hata hivyo, ili kutengeneza ndege hizo, angali eneo kubwa hilo linahitajika

Comments

Popular posts from this blog

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Je unayafahamu maajabu ya Ziwa Ngosi Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika inayozungukwa na vivutio vingi vya utalii na vingine inawezekana hata havitambuliwi na wenyeji. Ziwa Ngosi yawezekana kuwa ni miongoni mwa vivutio hivyo. Ziwa hili ambalo ni la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya ziwa lingine la kreta lililopo Ethiopia linaakisi muonekano wa bara la Afrika katika upande wa kusini, magharibi, kaskazini na mashariki pamoja na visiwa vyake vya Unguja na Pemba.

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...