Skip to main content

Uchaguzi DRC 2018: Kwa nini huenda Rais Joseph Kabila akawania urais tena 2023

  Bw Kabila Kinshasa 9 Desemba, 2018
 Bw Kabila anasema bado safari ni ndefu

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila amesema ataendelea kushiriki katika siasa nchini humo hata baada ya kuondoka madarakani baada ya uchaguzi utakaofanyika wiki mbili zijazo.
Aidha, hajafutilia mbali uwezekano wake wa kuwania tena urais uchaguzi mkuu mwingine utakapoandaliwa mwaka 2023.
Bw Kabila alitarajiwa kuondoka madarakani miaka miwili iliyopita baada ya kuongoza kwa mihula miwili kwa mujibu wa katiba.
Hata hivyo, uchaguzi mkuu nchini humo uliahirishwa mara kadha, serikali ikisema maandalizi yake hayakuwa yamekamilika vyema.
Upinzani ulitazama hilo kama njama ya Bw Kabila kutaka kuendelea kuongoza.

Mwezi Agosti, Bw Kabila alimtangaza mshirika wake wa karibu Emmanuel Ramazani Shadary ambaye ni waziri wa zamani wa mambo ya ndani kuwa mgombea wa muungano wa kisiasa unaotawala kwa sasa.
Bw Shadary amewekewa vikwazo na Umoja wa Ulaya kutokana na tuhuma za ukiukaji wa haki za kibinadamu.
Katibu wa chama cha upinzani cha Movement for the Liberation of Congo (MLC), Eve Bazaiba, ameambia BBC kwamba Bw Shadary atadhibitiwa na Bw Kabila na kwamba kimsingi itakuwa ndiye anayeongoza nchi.
"Anataka tu kusalia madarakani. Hata kama alimchangua Shadary, Shadary ni mtu tu wa kuonekana, ndiye atakayemuongoza Shadary kwa kila jambo. Kiuhalisia, atakuwa bado ndiye rais."
Bi Bazaida amesema serikali imekuwa ikiwazuia wanasiasa wa chama cha MLC kufanya kampeni.
Emmanuel Ramazani Shadary
Kwa muda mrefu, ilikuwa bado haijabainika iwapo Rais Kabila, angewania tena hadi alipoamua kumtangaza Shadary kuwa mgombea wa muungano wake wa kisiasa.

Kwenye mahojiano na shirika la habari la Reuters, Rais Kabila amesema: "Mbona tusisubiri hadi mwaka 2023 … ndipo tuwe na uwazi kuhusu mambo haya," alisema.
"Maishani sawa na ilivyo katika siasa, hauwezi kufutilia mbali jambo kabisa."
Kumekuwa na wasiwasi kutoka kwa upinzani na jamii ya kimataifa kuhusu iwapo uchaguzi wa DRC utakuwa huru na wa haki.
Lakini Bw Kabila amesema wasiwasi huo haufai kuwepo.
Martin Fayulu Novemba 11, 2018 Geneva
 Martin Fayulu awali alitangazwa kuwa mgombea wa muungano wa upinzani


"Tunakusudia kadiri ya uwezo wetu kuhakikisha uchaguzi huu hauna kasoro hata moja. Waangalizi wanaofikiria kwamba uchaguzi huu hautakuwa huru na wa haki, bado sijawaona wakija hapa na kusema ni kitu gani tumekikosa."
Kabila aliingia madarakani akiwa na miaka 29 baada ya babake Laurent Desire Kabila kuuawa na mlinzi wake mwaka 2001.
Aliahidi kurejesha amani na kuangamiza ufisadi na amekuwa akitaja hayo kama baadhi ya mafanikio ya utawala wake.

DRC ilikuwa imekabiliwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya mwaka 1998 na mwaka 2003 ambapo takriban watu 5 milioni walifariki kutokana na vita, njaa na maradhi.
"Tuna majuto yoyote? La hasha, hata kidogo. Tumepata mafanikio mengi. Jambo kuu zaidi ni kwamba tuliweza…kuliunganisha tena taifa na kulirejesha kwenye mkondo ufaao."
Kabila amesema anataka kusalia katika siasa ili kulinda mafanikio hayo na kuongeza kwamba wanaotaka kutoa uamuzi kuhusu mafanikio yake wanaweza kusubiri hadi amalize kazi yake.
"Bado kuna safari ndefu sana mbele yetu na kuna sura nyingi sana ambazo zitaandikwa kabla tuanze kuandika vitabu vya historia."
Vital Kamerhe (kushoto) na Felix Tshisekedi
 Felix Tshisekedi ameungana na Vital Kamerhe ambaye ni mgombea mwenza wake

Katiba nchini DRC inamzuia mtu aliyeongoza kwa mihula miwili mfululizo kuwania tena urais, lakini haijazuia mtu kama huyo kuwania tena baada ya kiongozi mwingine kuingia madarakani.
Baadhi wanasema huenda kikawa kisa kama cha rais wa Urusi Vladimir Putin ambaye baada ya kuongoza kama rais kati ya 2000 na 2008, alikuwa waziri mkuu kati ya 2008 na 2012 kabla ya kurejea tena kama rais wa nchi hiyo. Alibadilishana na mwandani wake Dmitry Medvedev ambaye kwa sasa ndiye waziri mkuu.

Comments

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...