Skip to main content

Zainab Mughal: Anategemea kuchangiwa damu ili apone saratani

zainabHaki miliki ya pichaONEBLOOD
Msichana mwenye umri wa miaka miwili huko nchini Marekani anahitaji kuchangiwa damu mara kadhaa ili kukabiliana na ugonjwa wa saratani.
Hali yake imegusa nyonyo za watu wengi, kampeni ya kuwatafuta wachangiaji damu inayofanana na ya mtoto huyo.
Zainab Mughal ni mtoto mwenye damu ya aina ya kipekee duniani ambayo inampa wakati mgumu kupata matibabu ya ugonjwa wake.
Waratibu wa kampeni hiyo wanasema zaidi ya watu 1,000 wamefanyiwa majaribu , lakini mpaka sasa ni watu watatu pekee ndio wenye damu inayohitajika .
Madaktari wanasema bado watahitajika wachangiaji kati ya saba hadi 10 ili kuweza kumtibu saratani yake .
Mapema mwaka huu Zainab aligundulika kuwa na saratani ya 'neuroblastoma', ambayo hujitokeza mara chache na kuathiri zaidi watoto .
Aidha kwa mujibu wa kituo cha damu 'Oneblood' kimebainisha kuwa uhamisho wa damu utahitajika kwa kipindi chote cha matibabu yake, lakini damu ya Zainab ni "nadra sana" kupatikana kwa sababu imekosa vimelea vya kundi 'B' ambavyo watu wengi huwa navyo katika seli zao za damu nyekundu.
Pia imebainika kuwa wachangiaji damu ambao wataweza kuendana na damu yake ni watu wenye asili ya Wapakistan ,Wahindi ama Wairan ambao wana aina ya damu ya kundi O na A.
zainabHaki miliki ya pichaCBS
Image captionZainab akiwa na baba yake na mama yake
Lakini hata katika idadi fulani ya watu wa Marekani , chini ya asilimia 4 hukosa vimelea hivyo vya kundi B.
Hata hivyo mwili wa Zainab utakataa damu yoyote ambayo itakuwa haijakidhi viwango vyote.
Wachangia damu wawili wenye damu zinazoendana naye tayari wamekwisha patikana nchini Marekani, ambapo mwingine mmoja amepatikana nchini Uingereza.
Kiongozi wa maabara katika kituo cha OneBlood, Frieda Bright, ameshangazwa sana kwani amekuwepo kwa miaka ishirini kwenye taaluma hii lakini hii ni mara ya kwanza kujitokeza kwa tatizo kama hilo.
Kituo hiko cha asasi isiyokuwa ya kiserikali, OneBlood hufanya kazi na mabenki mengine ya damu pamoja na Programu ya kutafuta wachangiaji damu Marekani 'ARDP'ambayo husaidia zaidi kupata wachangiaji wenye damu za kipekee duniani.
"Licha ya kuwa damu haitamponya lakini ni muhimu sana kuipata ili apate matibabu ya saratani, "Bi Bright amesisitiza katika video ya kampeni hiyo.
Baba yake Zainab ,Raheel Mughal alisema kuwa binti yake aligundulika na ugonjwa huo mwezi Septemba mwaka huu.
damu
Anasema walilia sana kwani jambo hilo hawakuwahi kutarajia kama litatokea.
Yeye na mama wa mtoto huyo walijitolea kutoa mchango wa damu zao wenyewe lakini madaktari waligundua kuwa hakuna hata mmoja ambaye ana damu inayoendana na ya Zainab.
Walitafuta watu wengi katika familia yao bila mafanikio na walipoenda kuchangisha damu kwa watu wengi zaidi ndio watu wakawa na taarifa zaidi .
Kwa mujibu wa kituo cha OneBlood wanasema matibabu ya kutumia mfumo wa mionzi tayari imekwisha kupunguza ukubwa wa tatizo la saratani.
mtotoHaki miliki ya pichaONEBLOOD
"Maisha ya binti yangu yanategemea damu.
Nimeshangazwa sana na jinsi wachangiaji damu wanavyoangaika kuokoa maisha ya binti yangu na kwa kazi wanayofanya sitoweza kuwasahau daima", Mughal alisema

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...