Skip to main content

Grace Mugabe anashutumiwa kumjeruhi mwanamitindo nchini Afrika Kusini

 Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkewe Grace mjini Harare, Zimbabwe,mwezi Julai 29, 2018
Waendesha mashtaka nchini Afrika Kusini wametoa waranti ya kukamatwa kwa mke wa Rais wa zamani wa Zimbabwe,Grace Mugabe, kutokana na tuhuma za kumshambulia mwanamitindo mwaka 2017, Polisi wameeleza.
Hatua hiyo imekuja baada ya mahakama kuibatilisha kinga yake ya kidiplomasia mwezi Julai.
Serikali ya Afrika Kusini ilikosolewa kwa kuruhusu Bibi Mugabe kuondoka nchini humo baada ya mashambulizi.
Gabriella Engels alimshutumu kwa kumpiga katika chumba cha hoteli mjini Johannesburg.
Msemaji wa polisi,Vishnu Naidoo amesema ''Siwezi kuthibitisha kuwa hati ya kumkamata Grace Mugabe ilitolewa Alhamisi iliyopita''.
Alisema polisi wanatafuta usaidizi kutoka idara ya Interpol kufanyia kazi waranti hiyo.
Haijafahamika kwa nini ripoti kuhusu waranti hiyo ilicheleweshwa na hakuna tamko lolote lililotolewa na Bibi Mugabe au mamlaka za Zimbabwe.
Familia ya Mugabe inamiliki mali nchini Afrika Kusini
Tukio la mashambulizi dhidi ya mwanamitindo lilitokea miezi mitatu kabla jeshi halijachukua mamlaka nchini Zimbabwe, hatua iliyomfanya Mugabe kujiuzulu baada ya kuwa madarakani kwa miaka 37.
Waandamanaji

Kilichotokea Johannesburg
Shambulio linaelezwa kutokea mwezi Agosti mwaka 2017 baada ya Bibi Mugabe kumkuta bi Engels akiwa na wanae wa kiume wawili, Robert na Chatunga katika chumba cha hoteli .
Wakati huo Bibi Mugabe alikuwa nchini Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu ya enka yake, vyombo vya habari vya Zimbabwe viliripoti.
Engels aliweka picha mtandaoni akionyesha jeraha la kichwani. ''Wakati Grace alipoingia hakujua yeye ni nani,'' alikiambia kituo cha News 24 cha Afrika Kusini.

''Aliingia na waya wa umeme na kuanza kunipiga nao, tena na tena.Sikujua kinachoendelea.Nilihitaji kutambaa kutoka nje kabla ya kukimbia.''
Aliongeza:''Kulikua na damu kila mahali.Mikononi, kichwani, kila mahali.''
Idara ya Polisi Afrika Kusini ilifanyia uchunguzi madai hayo lakini waziri wa mambo ya nje wakati huo, Maite, Nkoana-Mashabane, alimpa kinga ya kidiplomasia bibi Grace, kumruhusu kuondoka nchini humo bila kujibu maswali yeyote.Kinga ambayo ilibatilishwa mwezi Julai.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...