Skip to main content

Fastjet: Shirika la ndege lapewa makataa kujieleza kwa nini wasifungiwe Tanzania

FastJet
Shirika la ndege la Fastjet Airlines Limited maarufu kama Fastjet Tanzania limepewa makataa ya siku 28 kueleza sababu zinazoweza kuzuialisifungiwe kuendelea kuhudu Tanzania.
Kwa mijibu wa Mamlaka ya Safari za Anga Tanzania, shirika la ndege la Fastjet limekosa sifa ya leseni ya usafiri wa anga kwa sababu halina ndege zozote kwa sasa.
TCAA imesema ilitoa notice ya siku 28 ya kulitaka shirika hilo lisitishe mauzo kwa abiria. Na limeamuru shirika hilo kurejesha pesa kwa abiria hao au kuwatafutia usafiri katika mashirika mengine.
Mamlaka hiyo pia imeamuru waliopata hasara wafidiwe kwa mujibu wa sheria, na watoe mpango mkakati kwa nini wasifutiwe leseni ndani ya siku 28, pia ikitokea shirika hilo limefungwa basi walipe stahiki za wafanyakazi.
Fastjet tayari wametangaza kusitisha safari zake zote za mwezi Desemba na mwezi Januari. Na wameahidi kurejesha nauli za abiria wote kuanzia tarehe 20 mwezi desemba mwaka 2018.
Katika taarifa yao kwa umma Fastjet wameomba radhi kwa wateja wao bila kuweka wazi utaratibu wa awali kwa hifadhi za wateja hao mpaka watakapo rejeshewa nauli siku chache zijazo.
BBC ilizungumza na mmiliki wa shirika la Fastjet Tanzania Lawrence Masha siku chache zilizopita ambapo aliomba radhi kwa wateja wapya na kufafanua kuwa anafanya awezalo kuingiza ndege nchini.

"Nawaomba radhi sana wateja wangu na malalamiko yao nadhani yataendelea kwa siku moja au mbili. Na nimeingia gharama ya kuingiza ndege nyingine ili kuweza kuwahudumia na nitaingiza ndege ya pili," Bw Masha aliambia BBC.
"Lazima ieleweke kwamba Fastjet PLC ambayo ndio iliyokuwa mmiliki wa Fastjet tanzania wao walikuwa hawana ndege, mimi sijanunua shirika ambalo lilikuwa na ndege nimenunua shirika ambalo lilikuwa na haki ya kutua.
"Kazi yangu ni kuhakikisha naleta ndege ambazo zinaweza kubeba abiria waliopo."
Hata hivyo mmiliki huyo ambaye amenunua asilimia 68 ya hisa za shirika hilo la ndege hivi karibuni ana changamoto kubwa ya kuhakikisha anaingiza ndege hizo alizoahidi kununua kabla Mamlaka ya anga TCAA haijawapokonya kibali.
Katika msimu huu wa sikukuu ambapo idadi ya wasafiri huongezeka, shirika hilo limeacha abiria wake solemba katika mikoa mbali mbali kama vile Dar es salaam na Mwanza huku baadhi ya abiria wakionekana kulalamika katika vyombo vya habari vya ndani na mitandao ya kijamii.
Shirika la Fastjet lilianza kupata mushikeli wa kifedha baada ya mmiliki wa awali Fastjet PLC aliyekuwa na asilimia 49 kujiondoa ambapo shirika hilo liliuzwa kwa wawekezaji wa ndani.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2011 likifahamika kama Fly540 Tanzania, lakini baada ya kununuliwa kikamilifu na Fly540 mwaka 2012, lilibadilishwa jina na kuwa Fastjet Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Je unayafahamu maajabu ya Ziwa Ngosi Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika inayozungukwa na vivutio vingi vya utalii na vingine inawezekana hata havitambuliwi na wenyeji. Ziwa Ngosi yawezekana kuwa ni miongoni mwa vivutio hivyo. Ziwa hili ambalo ni la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya ziwa lingine la kreta lililopo Ethiopia linaakisi muonekano wa bara la Afrika katika upande wa kusini, magharibi, kaskazini na mashariki pamoja na visiwa vyake vya Unguja na Pemba.

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...