Skip to main content

Fastjet: Shirika la ndege lapewa makataa kujieleza kwa nini wasifungiwe Tanzania

FastJet
Shirika la ndege la Fastjet Airlines Limited maarufu kama Fastjet Tanzania limepewa makataa ya siku 28 kueleza sababu zinazoweza kuzuialisifungiwe kuendelea kuhudu Tanzania.
Kwa mijibu wa Mamlaka ya Safari za Anga Tanzania, shirika la ndege la Fastjet limekosa sifa ya leseni ya usafiri wa anga kwa sababu halina ndege zozote kwa sasa.
TCAA imesema ilitoa notice ya siku 28 ya kulitaka shirika hilo lisitishe mauzo kwa abiria. Na limeamuru shirika hilo kurejesha pesa kwa abiria hao au kuwatafutia usafiri katika mashirika mengine.
Mamlaka hiyo pia imeamuru waliopata hasara wafidiwe kwa mujibu wa sheria, na watoe mpango mkakati kwa nini wasifutiwe leseni ndani ya siku 28, pia ikitokea shirika hilo limefungwa basi walipe stahiki za wafanyakazi.
Fastjet tayari wametangaza kusitisha safari zake zote za mwezi Desemba na mwezi Januari. Na wameahidi kurejesha nauli za abiria wote kuanzia tarehe 20 mwezi desemba mwaka 2018.
Katika taarifa yao kwa umma Fastjet wameomba radhi kwa wateja wao bila kuweka wazi utaratibu wa awali kwa hifadhi za wateja hao mpaka watakapo rejeshewa nauli siku chache zijazo.
BBC ilizungumza na mmiliki wa shirika la Fastjet Tanzania Lawrence Masha siku chache zilizopita ambapo aliomba radhi kwa wateja wapya na kufafanua kuwa anafanya awezalo kuingiza ndege nchini.

"Nawaomba radhi sana wateja wangu na malalamiko yao nadhani yataendelea kwa siku moja au mbili. Na nimeingia gharama ya kuingiza ndege nyingine ili kuweza kuwahudumia na nitaingiza ndege ya pili," Bw Masha aliambia BBC.
"Lazima ieleweke kwamba Fastjet PLC ambayo ndio iliyokuwa mmiliki wa Fastjet tanzania wao walikuwa hawana ndege, mimi sijanunua shirika ambalo lilikuwa na ndege nimenunua shirika ambalo lilikuwa na haki ya kutua.
"Kazi yangu ni kuhakikisha naleta ndege ambazo zinaweza kubeba abiria waliopo."
Hata hivyo mmiliki huyo ambaye amenunua asilimia 68 ya hisa za shirika hilo la ndege hivi karibuni ana changamoto kubwa ya kuhakikisha anaingiza ndege hizo alizoahidi kununua kabla Mamlaka ya anga TCAA haijawapokonya kibali.
Katika msimu huu wa sikukuu ambapo idadi ya wasafiri huongezeka, shirika hilo limeacha abiria wake solemba katika mikoa mbali mbali kama vile Dar es salaam na Mwanza huku baadhi ya abiria wakionekana kulalamika katika vyombo vya habari vya ndani na mitandao ya kijamii.
Shirika la Fastjet lilianza kupata mushikeli wa kifedha baada ya mmiliki wa awali Fastjet PLC aliyekuwa na asilimia 49 kujiondoa ambapo shirika hilo liliuzwa kwa wawekezaji wa ndani.
Shirika hilo lilianzishwa mwaka 2011 likifahamika kama Fly540 Tanzania, lakini baada ya kununuliwa kikamilifu na Fly540 mwaka 2012, lilibadilishwa jina na kuwa Fastjet Tanzania.

Comments

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...