Skip to main content

Burundi: Rais Pierre Nkurunziza asema Rwanda imekuwa adui, ataka kikao cha EAC kiandaliwe

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza
Image captionRais wa Burundi Pierre Nkurunziza
Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza amesema kuna mzozo wa wazi kati ya taifa lake na taifa jirani na Rwanda katika kinachoonekana kuwa kudorora zaidi kwa uhusiano baina ya mataifa hayo mawili.
Rwanda na Burundi zimekuwa na uhasama kwa muda sasa, Burundi ikiituhumu Rwanda kwa kuhusika katika jaribio la kupindua serikali mwaka 2015 ambalo lilifeli.
Burundi hudai kwamba Rwanda iliwafadhili waliohusika na kwamba inatoa hifadhi kwao. Rwanda mara kwa mara imekuwa ikikanusha tuhuma hizo.
Rais Nkurunziza amemwandikia barua mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Yoweri Museveni ambaye ni rais wa Uganda akisema Rwanda sasa si mshirika tena ndani ya jumuiya bali ni kama adui.
"Rwanda ndiyo nchi pekee katika kanda hii ambayo ndiyo moja wa wahusika wakuu katika kuvuruga uthabiti wa taifa langu na kwa hivyo siichukulii kama taifa mshirika, lakini kama adui ya nchi yangu," barua hiyo, ambayo inaonesha ilitiwa saini na Bw Nkurunziza tarehe 4 Desemba, imesema.
Kiongozi huyo anataka kufanyike mkutano maalum wa EAC wa kujadili mzozo huo kati ya Rwanda na Burundi.
Viongozi wa mataifa ya jumuiya hiyo ambayo kwa sasa inajumuisha Burundi, Rwanda, Uganda, Kenya, Tanzania na Sudan Kusini wamepangiwa kukutana tena 27 Desemba.
Hii ni baada ya mkutano wao wa karibuni zaidi kukosa kuendelea jijini Arusha kutokana na kutokuwepo kwa ujumbe kutoka Burundi.
Burundi
Burundi inasisitiza kwamba Rwanda ndiyo chanzo kikuu cha machafuko yaliyotokea Burundi tangu Aprili 2015, na kwamba mzozo huo ulianza mapema mwaka 2010 baadhi ya makundi ya upinzani yalipoanza kusema kwamba hakungekuwa na uchaguzi 2015.
Burundi inadai kwamba Rwanda imekuwa ikihusisha katika visa vya utovu wa amani Rwanda, ikishirikiana na mkoloni wa zamani Ubelgiji.
"Rwanda ilikataa kushirikiana na kundi la pamoja la kutathmini hali halisi lakini Burundi ilishirikiana kikamilifu, na huu ni ushahidi tosha kwamba taifa hilo halijawahi kutaka ukweli ufahamuke kwa sababu ya uchokozi wake dhidi ya Burundi.
"Ni wazi kwamba Jumuiya ya Afrika Mashariki haifai kufumbia macho mateso haya yanayowakuta wana wa Burundi."
Burundi imesema kamwe haitakubali pendekezo la jumuiya ya kimataifa la kuruhusu vikosi kutoka nje kudumisha amani Burundi na kutolewa kwa msamaha kwa wanaodaiwa kuhusika katika jaribio la mapinduzi ya serikali ya mwaka 2015 kama masharti kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa mwaka 2020.
Barua hiyo inasema kukubaliwa kwa mapendekezo hayo kutakuwa ni ukiukaji wa sheria za Burundi.
"Wahusika katika mapinduzi ya serikali kote huwajibishwa na kushtakiwa katika mahakama na majopo ya mahakama, kwa nini basi hawa wa Burundi iwe tofauti kwao?," barua hiyo inasema.
"Nasikitika, Mheshimiwa Rais (Bw Museveni) kukufahamisha kwamba kamwe sitaketi meza moja na wahusika wa mapinduzi…ninapendekeza kuandaliwa kwa kikao maalum cha viongozi wa mataifa ambacho ajenda yake itakuwa kutatua suala la mzozo wa wazi kati ya Burundi na Rwanda," amesema Bw Nkurunziza kwenye barua hiyo.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...