Skip to main content

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn



Jacqueline NtuyabaliweHaki miliki ya pichaJACQUELINE NTUYABALIWE 

Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania.
Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000).
Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd .
Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi.
Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani.
Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike
Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu

Muziki

Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites.
Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu.
Mnamo mwaka 2004 alitoa kibao chake 'Nalia kwa Furaha'. akimshirikisha Bushoke
Mwaka 2007 alitoa albamu nyengine kwa jina 'Crazy over You' akimshirikisha Squeezer ambacho kilikuwa kibao cha kwanza cha albamu yake mpya.
Pia aliimba 'Nipe Mkono' akimshirikisha Mr Blue
Anasema kwamba umaarufu wake ulianza alipoanza kuimba
Kulingana na mjasiriamli huyo muziki ndio uliokuwa ndoto yake kubwa akiwa mtoto .
Alitizama kanda za video za wanamuziki tajika kama vile Mariah Carey na Whitney Houston ili kujifunza kuimba

Malkia wa urembo

2000 Alichaguliwa malkia wa Urembo nchini Tanzania baada ya kushinda taji la malkia wa urembo la miss Ilala.
Alitumikia taji la miss Tanzania kwa mwaka mmoja akizishughulikia jamii mbalimbali
Katika kushiriki katika shindano hilo alishawishiwa na mmoja wa waandalizi wa shindano hilo kujaribu bahati yake.
Katika shindano la dunia lililofanyika nchini Uingereza , alikutana na watu tofauti waliokuwa na malengo tofauti ambapo anadai kujifunza mambo mengi tofauti

Tuzo alizoshinda

2007: Alishinda tuzo ya mwanamuziki bora wa kike pamoja Tanzania na kolabo bora kupitia wimbo wake Crazy over you
2007: Alishinda tuzo ya Mwanamuziki bora kutoka Pearl Music Award
2008: Alishinda tuzo nyengine ya mwanamuziki bora wa Tanzania
2008: Alipata tuzo ya Mwanamuziki bora wa kike Tanzania kutoka Pearl Music Awards
2013: Alishinda taji la mwanamke mwenye mitindo bora katika tuzo za fesheni za Swahili
2017: Alijishindia tuzo ya shaba ya kimatifa kwa jina, Sayari amp,
2017: Alijishindia tuzo nyengine ya shaba katika orodha ya samani kwa jina Ngorongoro settee,

Ndoa

Mwaka 2015 alifunga ndoa na Bilionea wa Tanzania Reginald Mengi, na wamejaliwa watoto wawili wavulana .
Marehemu mumewe ni mwenyekiti wa makampuni ya IPP nchini Tanzania

Comments

Popular posts from this blog

Je unayafahamu maajabu ya Ziwa Ngosi Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika inayozungukwa na vivutio vingi vya utalii na vingine inawezekana hata havitambuliwi na wenyeji. Ziwa Ngosi yawezekana kuwa ni miongoni mwa vivutio hivyo. Ziwa hili ambalo ni la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya ziwa lingine la kreta lililopo Ethiopia linaakisi muonekano wa bara la Afrika katika upande wa kusini, magharibi, kaskazini na mashariki pamoja na visiwa vyake vya Unguja na Pemba.

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...