Skip to main content

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn



Jacqueline NtuyabaliweHaki miliki ya pichaJACQUELINE NTUYABALIWE 

Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania.
Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000).
Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd .
Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi.
Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani.
Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike
Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu

Muziki

Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites.
Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu.
Mnamo mwaka 2004 alitoa kibao chake 'Nalia kwa Furaha'. akimshirikisha Bushoke
Mwaka 2007 alitoa albamu nyengine kwa jina 'Crazy over You' akimshirikisha Squeezer ambacho kilikuwa kibao cha kwanza cha albamu yake mpya.
Pia aliimba 'Nipe Mkono' akimshirikisha Mr Blue
Anasema kwamba umaarufu wake ulianza alipoanza kuimba
Kulingana na mjasiriamli huyo muziki ndio uliokuwa ndoto yake kubwa akiwa mtoto .
Alitizama kanda za video za wanamuziki tajika kama vile Mariah Carey na Whitney Houston ili kujifunza kuimba

Malkia wa urembo

2000 Alichaguliwa malkia wa Urembo nchini Tanzania baada ya kushinda taji la malkia wa urembo la miss Ilala.
Alitumikia taji la miss Tanzania kwa mwaka mmoja akizishughulikia jamii mbalimbali
Katika kushiriki katika shindano hilo alishawishiwa na mmoja wa waandalizi wa shindano hilo kujaribu bahati yake.
Katika shindano la dunia lililofanyika nchini Uingereza , alikutana na watu tofauti waliokuwa na malengo tofauti ambapo anadai kujifunza mambo mengi tofauti

Tuzo alizoshinda

2007: Alishinda tuzo ya mwanamuziki bora wa kike pamoja Tanzania na kolabo bora kupitia wimbo wake Crazy over you
2007: Alishinda tuzo ya Mwanamuziki bora kutoka Pearl Music Award
2008: Alishinda tuzo nyengine ya mwanamuziki bora wa Tanzania
2008: Alipata tuzo ya Mwanamuziki bora wa kike Tanzania kutoka Pearl Music Awards
2013: Alishinda taji la mwanamke mwenye mitindo bora katika tuzo za fesheni za Swahili
2017: Alijishindia tuzo ya shaba ya kimatifa kwa jina, Sayari amp,
2017: Alijishindia tuzo nyengine ya shaba katika orodha ya samani kwa jina Ngorongoro settee,

Ndoa

Mwaka 2015 alifunga ndoa na Bilionea wa Tanzania Reginald Mengi, na wamejaliwa watoto wawili wavulana .
Marehemu mumewe ni mwenyekiti wa makampuni ya IPP nchini Tanzania

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wafungwa wa Guantanamo Bay wawasili Saudi Arabia

Kundi la wafungwa wa Yemen waliozuiliwa nchini Marekani katika Gereza la Guantanamo Bay wamewasili nchini Saudi Arabia. Waandishi kutoka katika shirika la habari la AFP wamesema watu watatu wameonekana wakipokelewa na familia zao katika uwanja wa ndege ambao kwa kawaida hupokea viongozi Mashuhuri katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Riyadh. Kuhamishwa kwa wafungwa kumetokea siku mbili baada ya Ikulu ya Marekani kuahidi kuendelea na mpango wake wa kuhamisha wafungwa kutoka kataka Gereza la Guantanamo Bay, wakipinga suala ambalo limekuwa likipingwa vikali na Rais mteule wa Marekani Donald Trump.