Skip to main content

George HW Bush:Mbwa wa rais zamani wa Sully agusa wengi kwa heshima zake za mwisho

Mbwa Sully akiwa amelala karibu na jeneza lenye mwili wa George HW BushHaki miliki ya pichaOFFICE OF GEORGE HW BUSH
Image captionPicha ya kwanza ya Mbwa Sully akiwa amelala karibu na jeneza lenye mwili wa George HW Bush iliyowagusa wengi
Mbwa huyo wa jina Sully alisindikiza jeneza hilo muda wote.
Picha ya kwanza kabisa ya Sully akitoa heshima zake ilipakiwa mtandaoni na msemaji wa Bw Bush Jim McGrath, pamoja na ujumbe: "Mission complete."
Sully the dog boarding Air Force OneHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionSully alisafiri na Air Force One iliyoubeba mwili wa marehemu kwenda Washington Jumatatu
Watu katika mitandao ya kijamii wamekuwa wakimshukuru Sully kwa huduma zake, na kwa kawaida kuzungumzia uaminifu wa mbwa kwa wamiliki wao.
Sully akiabiriAir Force OneHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionAlirejea vivyo hivyo Texas Jumatano
Sully amepewa jina la rubani wa ndege za abiria Chesley "Sully" Sullenberger, ambaye alifanikiwa kuielekeza ndege ya kubeba abiria kutua kwa dharura kwenye Mto Hudson mwaka 2009, na kuwaokoa abiria wote 155 na wahudumu waliokuwa kwenye ndege hiyo.
Mbwa huyo mwenye miaka miwili alikabidhiwa jukumu la kuwa mbwa msaidizi wa Bush aliyekuwa akitumia kiti cha magurudumu mapema mwaka huu.
Sully ni mbwa aliyepokea mafunzo sana, na anaweza kutekeleza maagizo mengi, ikiwemo kufungua milango na kuchukua vitu vinavyohitajika na mmiliki wake, mfano simu inapoita.
Sasa atahudumu kama mbwa msaidizi kwa wanajeshi waliojeruhiwa vitani.
Sully ana ukurasa wake kwenye Instagram, na hapa anaoneshwa akimsaidia Bw Bush kupiga kura wakati wa uchaguzi wa katikati ya muhula mwezi jana.
Presentational white space
Sio marais wote wa Marekani wanaowapenda mbwa hata hivyo.
John F Kennedy hakuwapenda kamwe, na Donald Trump hana mbwa. Lakini Barack Obama anawapenda mbwa sana.
Obamas and BoHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionFamilia ya Obama na mbwa wao Bo mwaka 2009
Rais Bush amekuwa akipokea matibabu ya ugonjwa wa Parkinson na alilazwa hospitalini akiwa na tatizo la maambukizi kwenye damu mwezi Aprili.
Alifariki akiwa na miaka 94 mjini Houston, Texas.
Atazikwa kwenye maktaba ya rais Texas, karibu na mkewe, Barbara Bush, aliyefariki dunia miezi saba iliyopita.

Comments

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...