Skip to main content

WHO: Idadi ya vijana wanaokufa kwa ajali za barabarani inazidi ya wanaokufa kwa virusi vya Ukimwi

ajaliHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Ajali za barabarani zinatajwa kuwa ndio zinasababisha vifo vingi vya watoto na vijana duniani, kwa mujibu wa shirika la afya duniani(WHO).
Shirika hilo la afya limechapisha ripoti ambayo inabainisha kwamba bara la Afrika ndilo lina ajali nyingi za barabarani duniani.
Katika taarifa nyingi zinasema kwamba waafrika na wamarekani wa Kusini bado hawana sheria nzuri za kudhibiti mwendo kasi.
Lakini taarifa hizo zimesisitiza kwamba vifo vinavyotokana na ajali za barabarani duniani huwa zinalingana na kiwango cha idadi ya watu.
Ajali za magari ndio zinaongoza duniani kusababisha vifo kwa watoto na vijana wenye umri kati ya miaka mitano mpaka 29, ripoti hiyo imesema.
Ripoti hiyo pia imeeleza kwamba watu wengi zaidi wanakufa kutokana na ajali za barabarani kuliko virusi vya ukimwi , kifua kikuu au magojwa ya kuhara.
"Vifo hivyo havikubaliki, hakuna sababu inayoweza kutetea matukio hayo .Hili ni tatizo ambalo linaweza kutafutiwa ufumbuzi" Mkurugenzi wa WHO alisema.
RIPOTI
Ripoti ya Shirika la afya duniani inasema kwamba kuna vifo 27 kwa kila watu 1000 . Vifo vya barabarani katika nchi za Afrika ni mara tatu zaidi ya ajali zinazotokea Ulaya, ambako kuna ajali chache zaidi.
Imesema ni karibu nusu ya mataifa 54 ya Afrika hayana sheria za mwendo kasi katika nchi zao.
Botswana, Ivory Coast na Cameroon, ni miongoni mwa nchi ambazo zimeona kiwango cha vifo vikiongezeka.
Egypt, Angola, Burkina Faso na Burundi ni miongoni mwa nchi ambazo wameshuhudia kuona ajali zikipungua.
RWANDA

Afrika ina kiwango kikubwa ya ajali ambazo zinasababisha vifo.

Kwa mujibu wa taarifa za hivi karibuni , zinasema kuwa watu milioni 1.35 waliuwawa katika ajali za magari duniani kwa mwaka 2016, kiwango ambacho kiko tofauti kidogo na mwaka uliopita.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...