Skip to main content

Faida tano za kimwili ambazo watu wachache wanazo

A DNA chainHaki miliki ya pichaISTOCK
Image captionKuna watu ambao wana vina saba ambavyo vinawafanya waweze kufanya vitu ambavyo watu wengine hawawezi.

Watu hao ambao wana uwezo wa ajabu wa kusadikika kama kwenye katuni na sayansi ya uongo.
Lakini baadhi ya binadamu wa kawaida tu huwa wana uwezo wa kipekee jambo ambalo kwa wengine ni ndoto tu kuwa na uwezo kama huo.
Katika baadhi ya kesi, huwa wanawakilisha vina saba ambavyo vilifanyiwa mabadiliko na kwa namna nyingine miili yao huwa inaonyesha inavyokubali aina fulani ya maisha.
Hii hapa ni mifano ya namna wanavyoweza wa kufanya mambo ambayo wengine hawawezi kufanya.

1.Kuwa na uwezo wa kuona vizuri ndani ya maji

Watu wengi hawawezi kuona vizuri wakiwa ndani ya maji.
Lakini watoto wa jamii ya Mokeni kutoka makabila matatu ya wanaishi pembezoni mwa pwani ya Myanmar na Thailand wanaweza kuona vizuri jambo ambalo si la kawaida.
Watu hawa wa kisiwani wanajulikana kama watu ambao wanahamahama na hutumia muda mwingi kuishi katika viota vilivyopo kwenye maji.
Kwa nini wana uwezo wa kuona vizuri wakiwa chini ya maji.
Hali hiyo inatokana na uwezo wa kisayansi wa namna ambavyo macho yanavyoweza kuangalia wakiwa hewani na kwenye maji.
A woman diving with her eyes openHaki miliki ya pichaISTOCK
Image captionTukifumbua macho tukiwa kwenye maji kwa kawaida hatuwezi kuona vitu vizuri
Kwenye hewa, mwanga huwa uko wazi, ingawa kiasi cha maji ambayo yanaweza kuingia katika macho kinafanana na majimaji yaliyoko kwenye macho, haiwezi kuonyesha muonekano mzuri .
Google ilitatua tatizo hili kwa kutengeneza mfuko wa hewa uliopo katikati ya jicho na maji.
Mwaka 2003, utafiti ulichapisha hali ya kibaiolojia kwa sasa inavyoonesha macho ya watoto wa jamii ya Moken wanavyoweza kuona wakiwa ndani ya maji kama vile vile pomboo anavyoweza kuona vizuri akiwa kwenye maji bila kubughudhiwa na kitu chochote.
Utafiti zaidi unaonyesha namna watu wazima wa jamii ya Moken ambao wengi ni wavuvi huwa wanapunguza uwezo huo wa kuona.
2. Kuvumilia maji baridi kupita kiasi
Binadamu huwa wanaweza kuimili joto la nyuzi joto kati 36.5 na nyuzi joto 37.5.
Na hii inaelezea namna ambavyo binadamu wana uwezo wa kuhimili joto kuliko baridi.
Lakini wahinuiti ambao wanaishi Arctic au Nenets ambao wanaishi magharibu ya Urusi wana uwezo wa kukaa kwenye baridi zaidi.
An Inuit man building an iglooHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Miili yao ina uwezo wa kuhimili hali tofauti ya baridi kwa sababu za kibailojia kuwa tofauti na sisi.
Ngozi zao zina joto zaidi ya kwetu na oganisimu zao ziko juu. Huwa wanatoa jasho kidogo na huwa hawatetemeki kwa baridi.
Tabia hii huwa inatokana na vina saba vyao hivyo kama wewe sio mtu kutoka Inuit au Nenet basi huwezi kuwa na uwezo kama waliokuwa nao wao wa kuweza kuhiili baridi hata kama ulihamia katika eneo lao kwa miongo kadhaa iliyopita.
3. Kulala kwa muda mfupi
Watu wengi huwa wanahitaji muda wa kulala kati ya saa saba mpaka nane kwa usiku mmoja ili waweze kupumzika.
Lakini mwaka 2014, utafiti wa wanachuo kutoka Marekani kuhusu dawa ya kulala umebaini kuwa kuna watu ambao wako tofauti na wana uwezo wa kufanya shughuli zao kama kawaida hata kama wakilala pungufu ya saa sita.
A man sleepingHaki miliki ya pichaISTOCK
Image captionWanasayansi wanashauri mtu alale kwa saa saba mpaka tisa kama una vina saba vya kawaida
Watu ambao wana vina saba ambavyo vina uwezo wa kuyafanya macho yao yafanye kazi vizuri na kufanya mapumziko yao mafupi yawe mazuri zaidi.
Upungufu wa muda wa kulala huwa unaathiri uwezo wa kuwa makini na kupelekea mtu kuwa na ugonjwa wa akili.
Aidha utafiti huo umesisitiza kuwa mabadiliko hayo huwa yanawatokea watu wachache sana , asilimia moja ya wale ambao wanadai kuwa huwa wanalala chini ya saa 6 kwa usiku mmoja.
Hivyo kama unalala pungufu ya saa sita na unadhani kuwa huwa unajisikia vizuri tu basi inabidi uwe makini.
Kuna kila namna ambayo ukosefu wa usingizi unaweza kukuletea madhara siku moja.
4. Mifupa yenye uzito mkubwa
Kupungua kwa ukubwa wa mifupa ni kitu cha kawaida kulingana na umri unavosogea lakini kuna watu wengine ambao huwa wanapungua uzito wa mifupa yao kwa haraka zaidi.
Hali ambayo inaweza kudhoofisha mifupa na kuongeza hatari ya kuweza kuathiri maisha ya mtu.
Wanasayansi kutoka Chiroscience Research and Development huko Bothell, nchini Marekani , jimbo la Washington, walibainisha namna ambavyo vina saba vinaathiri uzalishwaji wa protini ambayo inatengeneza mifupa .
SkeletonsHaki miliki ya pichaISTOCK
Wanasayansi hao wana matumaini kuwa ujuzi huu utawasaidia kupata njia ya kuondoa udhaifu wa mifupa kadri ya umri unavyoenda.
Lakini kuna athari zake pale ambapo mifupo inapoendelea kukua inaweza kuleta athari kiafya na kumfanya mtu ashindwe hata kusikia na kupata madhara katika muonekano wake pia.
Hali ya vina hivi huwa inapatika kwa watu wa asili ya Afrikaner kutoka Afrika kusini .

5. Kuweza kuishi katika kina kirefu cha maji

Jamii ya Andean, ambao wanaishi katika kina cha mita 5000 chini ya bahari, wanajulikana kama "soroche" na mtu yeyote ambaye amewahi kufika katika kina kirefu aina hiyo anaweza kujua namna hali inavyokuwa.
Unaweza ukaugua kwa kukosa okysijeni ambayo huwa inakuwa nadra kuipata kadri unavyokuwa chini ya bahari.
Dalili zake huwa zinaanza kwa kusikia kizunguzungu , kichwa kuuma, mapigo ya moyo na kupata shida kuhema.
Lakini utafiti uliofanywa katika Quechua ya Andes na Himalaya inaonyesha namna ambavyo kuna baadhi ya watu wanaweza kuishi katika kina hicho bila kupata tabu yeyote.
Kadri muda unavoenda huwa wanakuwa na kifua kikubwa kinachowawezesha kupumua kiurahisi muda wote.
Wakati watu wengi huwa wanazalisha chembe nyekundu katika miili yao ili ipokea oksijeni , ambayo inatengezwa.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Wafungwa wa Guantanamo Bay wawasili Saudi Arabia

Kundi la wafungwa wa Yemen waliozuiliwa nchini Marekani katika Gereza la Guantanamo Bay wamewasili nchini Saudi Arabia. Waandishi kutoka katika shirika la habari la AFP wamesema watu watatu wameonekana wakipokelewa na familia zao katika uwanja wa ndege ambao kwa kawaida hupokea viongozi Mashuhuri katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Riyadh. Kuhamishwa kwa wafungwa kumetokea siku mbili baada ya Ikulu ya Marekani kuahidi kuendelea na mpango wake wa kuhamisha wafungwa kutoka kataka Gereza la Guantanamo Bay, wakipinga suala ambalo limekuwa likipingwa vikali na Rais mteule wa Marekani Donald Trump.