Skip to main content

Chika Okafor, Onyeka Ufere na Ogechi Babalola: Dada watatu wa Nigeria walioshika mimba wakati mmoja Marekani

Pregnant Sisters
Huwa ni furaha kwa mwanamke kushika mimba na kujawa na matumaini ya kujifungua, na huwa kawaida kwa dada kumfichulia dadaki habari punde anapothibitisha.
Ogechi Babalola alikuwa na furaha kama hiyo alipogundua kwamba alikuwa ameshika mimba na angejifungua kifungua mimba wake.
Lakini alipokwenda kuwafichulia dada zake, kila mmoja aligundua kwamba alikuwa anabeba mimba.
Watatu hao, waliozaliwa Nigeria ingawa kwa sasa wanaishi Marekani, walipigwa picha kwa pamoja, wakiwa wajawazito, picha ambazo zimewavutia watu si haba mtandaoni - wengi wakifurahia pamoja nao.
Kwanza Ongechi alikwenda kwa Chika Okafor na kumfichulia habari.
Onyeka Ufere, 30, alipofahamishwa, naye akawafahamisha kwamba naye alikuwa mjamzito.
Mmoja wao, Chika Okafor ndiye aliyepakia picha hizo kwenye mtandao wa Instagram na kuongeza ujumbe: "Kama wanifahamu vyema, basi wafahamu kwamba huwa nawapenda sana dada zangu. Nimekuwa nikigawana nao karibu kila kitu (mavazi, walimu, wazazi, chakula). Sasa tutakuwa pamoja kwenye safari hii ya kusisimua ya kuwa mama. Mungu na wakati wake, ni kama mwujiza. Singefikiria hata wakati mmoja kwamba hili lingetokea."
Wameambia chombo kimoja cha habari kwamba hawakufahamu jinsi kisa chao kilivyokuwa cha kipekee.
Wote wameolewa, na wanatarajia kujifungua watoto wao wakiwa wameachana kwa wiki kadha tu.
"Kwangu na dadangu Chika, ulikuwa ni wakati wetu wa kwanza kushika mimba, na kwa hivyo wazo la kufanya hivi tukiwa peke yetu lilikuwa linatutia wasiwasi. Onyeka amepitia hili awali, ambapo alijaliwa watoto pacha," Babalola aliambia Yahoo Lifestyle.
Anasema hakuna kule kulalamika, kucheka na kusumbuka na kutokwa na machozi kwani katika kila analolipitia, anafahamu kwamba kuna mwenzake ambaye anapitia kitu sawa na hicho.
Babalola, 26, na Okafor, 27, wanatarajia kujifungua watoto wavulana.
Ufere, 30, anatarajia kujifungua watoto wengine pacha, lakini bado hajabaini jinsia yao.
Anatarajia kufahamu hilo Desemba.
Wanawake hao waliozaliwa Nigeria waliamua kupigwa picha za pamoja wakiwa wajawazito walipofahamu kwmaba dada yao mdogo alikuwa azuru California, jimbo walilokulia. Kwa sasa anaishi Atlanta.
Huo ulikuwa wakati wa kwanza kwao kukutana wakiwa wajawazito na hivyo wakaamua kuwa na kumbukumbu.
"Kwani ni mara ngapi mtapata tena fursa ya kuwa wajawazito kwa pamoja? Ni baraka ambayo lazima tuinakili," Okafor aliambia Yahoo Lifestyle.
Picha zilipigwa na rafiki yao Cynthia Onyejiji.
Dada hao wanatumai kwamba uhusiano wao wa karibu utaigwa na watoto wao.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...