Skip to main content

Waajiri China; wawalisha mende wafanyakazi kwa kushindwa kufikia lengo la biashara

Ukishindwa kufikia malengo ya kibiashara , basi mende kama huyo halali yakoWasimamizi katika kampuni ya Kichina wamefungwa jela kwa kuwaadhibu wafanyakazi walioshindwa kufikia malengo ya mauzo kibiashara kunywa mkojo na pia kula mende, vimearifu vyombo vya habari.
Polisi wamechukua hatua baada ya video kuowaonesha wafanyakazi hao wakichapwa kwa mkanda na kunywa kitu kioevu chenye rangi ya njano.
Mameneja watatu wamehukumiwa kifungo jela kati ya miaka mitano na kumi kutokana na tukio hilo, linaarifu gazeti la Morning Post limearifu.
Video hiyo imekuwa maarufu mitandaoni na watu kutumiana kwa wingi kwenye mitandao nchini China na tovuti mbali mbali ikiwemo tovuti ya Weibo iliyoweka video inayomuonesha muajiri wa kiume akiwa amesimama katikati ya mduara akipigwa mjeledi.
Video hiyo haraka sana ikawekwa kwenye tovuti ya WeiboHaki miliki ya pichaPEARVIDEO
Image captionVideo hiyo haraka sana ikawekwa kwenye tovuti ya Weibo
Wafanyakazi wengine, inaarifiwa kuwa ukiwa ni muajiriwa katika kampuni ya ukarabati majengo katika mji wa Guizhou, si ajabu kuonekana ukinywa kimiminika chenye rangi ya manjano kilichowekwa katika kijikombe cha plastiki huku ukiwa umebinya pua yako .
Ujumbe ulionaswa kwa picha uliosemekana kutoka kwa wasimamizi wa mgahawa huo, zilijaa vitisho kwa wafanyakazi kwamba watalazimika kula mende kutokana na uwajibikaji wao mdogo kikazi.
Kwa muujibu wa vyombo wa habari nchini humo, aina nyingine ya aibu na adhabu katika kampuni hiyo ni pamoja na kunywa maji ya kutawaza yaliyoko chooni ama maji ya siki na kunyoa vipara vichwa vyao.
Haki miliki ya picha
picha inayoonekana na vijikombe vidogo vili oneshwa kwenye mitandao ya jamii nchini humo na kuelezwa kuwa kimiminika hicho ni mkojo

picha inayoonekana na vijikombe vidogo vili oneshwa kwenye mitandao ya jamii nchini humo na kuelezwa kuwa kimiminika hicho ni mkojo

Polisi katika kata ya Zunyi waliwatia mbaroni mameneja watatu na baadaye kufuwahukumu kifungo cha maisha jela.
Katika siku za hivi karibu imekuwa ni mastaajabu kwa makampuni ya kichina kutumia adhabu kama hizo, kuadhirisha ama kuwatia moyo wafanyakazi wao.
Taarifa za hivi karibuni zinaarifu kuwa kumekuwa na mifano ya kesi kama hizo kwa wafanyakazi kupigana makofi wenyewe kwa wenyewe kwa lengo la kuongeza ari kazini, na wafanyakazi kulazimishwa kutambaa barabarani ama kubusu mapipa ya takataka kama adhabu au kuongeza mshikamano kazi.
Kampuni hiyo pia inaarifiwa kushindwa kuwalipa wafanyakazi wake mishahara kwa muda wa miezi miwili iliyopita, na wafanyakazi walikuwa na hofu ya kuzungumzia suala hilo kwa kuhofia kupoteza malipo yao enapo pia wataacha kazi

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...