Skip to main content

Je unayafahamu maajabu ya Ziwa Ngosi Tanzania

Ziwa Ngosi lina muonekano wa ramani ya AfrikaTanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika inayozungukwa na vivutio vingi vya utalii na vingine inawezekana hata havitambuliwi na wenyeji.
Ziwa Ngosi yawezekana kuwa ni miongoni mwa vivutio hivyo.
Ziwa hili ambalo ni la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya ziwa lingine la kreta lililopo Ethiopia linaakisi muonekano wa bara la Afrika katika upande wa kusini, magharibi, kaskazini na mashariki pamoja na visiwa vyake vya Unguja na Pemba.

Ziwa Ngosi linapatikana kwenye milima ya Uporoto, Mkoa wa Mbeya nyanda za juu kusini mwa Tanzania , ziwa hili linatajwa kutokana na mlipuko wa volkano hivyo ni tofauti na maziwa mengine kama ziwa victoria au ziwa nyasa.
Upekee au utofauti wa ziwa hili ni kwamba ziwa hili liko juu ya milima na katikati ya misitu na lina urefu wa km2.5, upana wake ni km 1.5 , kina chake ni mita 74 na lina ukubwa wa hecta 9332.
Muonekano wa bara la Afrika ambao upo katika ziwa la Ngosi ni sawa na mchoro unao onekana wa ramani ya bara la afrika pamoja na visiwa vyake uliopo kwenye jiwe kubwa lililopo mkoani Njombe, Kusini magharibi mwa Tanzania ambao haujachorwa na mwanadamu.

Innocent Lupembe ni mtaalamu wa misitu na mali asili katika wakala wa huduma za misitu nchini Tanzania kanda ya nyanda za juu kusini mwa Tanzania anasema hifadhi ya msitu wa mporoto ulianza kutunzwa mwaka 1937 kwa ajili ya kuhifadhi vyanzo vya maji,mimea pamoja na wanyama.
Msitu huu ni wa kipekee kwa sababu una ziwa ndani yake tofauti na misitu mingine na ili uweze kuliona ziwa ni lazima upande mlima ndio unaweza kuliona.
Ziwa hili halina mto unaoingiza wala kutoa maji, ni sawa na maji kwenye bakuli.

Kima cha maji hakibadiliki


ngosi
Ujazo wa maji huwa haubadiliki yani huwa hivyohivyo wakati wa masika au kiangazi na ujazo wa maji huwa haubadiliki.
Maajabu mengine katika ziwa hili ni kwamba maji ya Ziwa Ngozi huwa lina muonekano wa rangi tofauti tofauti kila wakati, kuna wakati ukifika unakuta ziwa lina rangi ya samawati , kijani au nyeusi .
Uwepo wa misitu husababisha rangi ya maji kubadilika na upande wa jua linapowaka"Lupembe alieleza .
Ndege hupendelea kuogelea pamoja na aina fulani ya bata huwa wanaogelea humo kwa wingi na kufanya ziwa kuwa na muonekano wa kupendeza zaidi.
Licha ya kuwa ziwa hilo linavutia kuangalia lakini halina samaki wala kuwa na historia ya uwepo wake na vilevile sio rafiki kwa kuogelea.

ngosi
Mtaalam wa hifadhi hiyo alibainisha kwamba miaka miwili iliyopita ziwa hilo liliweza kusababisha vifo vya watoto wawili ambao walikufa baada ya kujaribu kuogelea lakini kabla ya hapo hakuna mtu aliyeweza kujaribu kuogelea kutokana na eneo hilo kuaminika kiimani.
Lakini kwa sasa serikali ina mpango wa kuanzisha utalii wa kuogelea kwa maboti madogo madogo na kuwekeza zaidi kwa ajili ya utalii.
Serikali ya Tanzania ina mradi mkubwa wa umeme ambao unaendelea ingawa wanachipa nje ya mlima.
Hii ni kutokana kuwa katika ziwa hili kuna joto ardhi na linatoa maji moto kwa chini ingawa ziwa Ngosi lenyewe juu maji ni baridi lakini chini ni moto.
Kuna sehemu kadhaa katika mkoa huo wa Mbeya ambapo maji yanatoka ya moto kabisa mpaka mtu unaweza kuchemsha mayai na chanzo kinatoka katika ziwa ngosi.
Kwa sasa eneo hilo linatembelewa na wageni kutoka nje ya nchi zaidi ya wenyeji na wanafunzi wa shule huwa wanafika hapo kwa wingi kwa ajili ya kujifunza.

Wanakijiji wa eneo hilo wana imani juu ya ziwa ngosi


ngosi
Mwalingo Kisemba ni chifu ambaye ni diwani katika kata ya Inyala halmashauri ya wilaya ya Mbeya.
Yeye anasema katika kabila la wasafa waliliita ziwa Ngosi au Ligosi kwa sababu waliona ni kubwa sana na kiimani ya kisafa waliamini kwamba Mungu yupo huko na walikuwa wakija kufanya maombi ili mvua inyeshe.
Katika kabila lao, wao waliamini kuwa ni bwawa la ajabu kutokana na maji yake kuwa baridi juu na chini kuwa moto.
Kisemba aliongeza kwamba maji ya ziwa hilo yaliaminika kuwa ni dawa ya ngozi, na watu walikuwa wakipaka wanapona ugonjwa wa ngozi kitu ambacho kuna ambao wanaamini hivyo mpaka leo.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...