Skip to main content

Sahle-Work Zewde: Rais mpya wa Ethiopia asiye na 'meno'

Sahle-Work ZewdeTaarifa za Ethiopia kumchagua rais wa kwanza mwanamke zimepokelewa kwa shangwe kote barani Afrika, lakini swali ni; rais huyo ana mamlaka gani?
Katika Jamuhuri nyingi duniani cheo cha rais kinashikilia mamlaka yote ya kisiasa na kidola. Jina la rais linawakilisha nguvu na uwezo wa kufanya maamuzi ya mwisho kwa mujibu wa katiba.
Changamoto kubwa ya kisiasa duniani na hususan Afrika ni kuwaamini na kuwachagua wanawake katika nafasi kuu za kiuongozi. Na pale inapotokea mwanamke kuchaguliwa katika ofisi kuu ya nchi moja bara zima hushangilia na kupigia mfano.
Kuchaguliwa Bi Sahle-Work Zewde na wabunge kuwa rais wa Ethiopia ni habari nzuri katika harakati za kuwainua wanawake wa Afrika, lakini wengi walioshangilia ushindi wake nje ya Ethiopia hawafahamu ukomo wa mamlaka yake.Wengi wanamjumuisha Bi Zewde katika fungu moja na Bi Ellen Johnson Sirleaf, rais mstaafu wa Liberia na Bi Joyce Banda rais mstaafu wa Malawi.
Ingawa wote wanabeba jina la Rais, kimamlaka Bi Zewde hayupo sawa na wanawake hao wengine wawili.
Bi Zewde yupo sawa na rais mstaafu wa Mauritus Ameenah Gurib-Fakim. Urais wao ni wa kiitifaki, kwa kingereza huitwa ceremonial.
Nchini Ethiopia katiba yao ya mwaka 1995 imewekeza nguvu zote za kisiasa na kiutendaji kwa Waziri Mkuu.
Hivyo, kiuhalisia, Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Bw Abiy Ahmed ananguvu zaidi ya Rais wake Bi Zewde.
Ahmed ni mkuu wa serikali na Zewde ni mkuu wa nchi.
.
Ethipoia si nchi pekee yenye mfumo kama huo. Mauritius ni nchi nyengine ya Afrika inayotumia mfumo huo.
Duniani baadhi ya nchi zenye mfumo kama huo ni India, Ujerumani, Italia na Israeli.
Kiongozi mkuu anayefahamika zaidi wa Ujerumani ni Kansela Angela Markel na yeye ndiye mwenye mamlaka ya kuongoza serikali. Rais wa Ujerumani ambaye wengi nje ya nchi hiyo wanaweza kuwa hawajahi kumskia anaitwa Frank-Walter Steinmeier.
Kwa upande wa India mwenye mamlaka ya kiutendaji na maamuzi ya kiserikali ni Waziri Mkuu Narendra Modi. Rais wa India anaitwa Ram Nath Kovind.
Kwa upande wa Israeli mwenye hatamu za kuingoza serikali ni Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu. Rais wa nchi hiyo ni Reuven Rivlin.
Katika mfumo huo, miongoni mwa kazi za rais ambaye ni mkuu wa nchi ni kuishauri serikali inayoongozwa na Waziri Mkuu na baraza la mawaziri. Kutangaza hali ya vita baada ya kushauriwa na bunge, kupokea hati za mabalozi wa kigeni, kuitisha uchaguzi na kutaja jina la mshindi wa uwaziri mkuu.
Rais pia hukubali na kutangaza kujiuzulu kwa waziri mkuu na serikali pale hali hiyo inapotokea.
Kwa baadhi ya nchi zenye mfumo wa kifalme, cheo na madaraka ya rais wa Ethipoia huwa ni ya Malkia ama Mfalme. Mfano mzuri ni Uingereza ambapo malkia Elizabeth ni mkuu wa nchi na Waziri Mkuu Bi Theresa May ni kiongozi wa serikali na hivyo mamlaka yote ya kiutawala wa dola yapo chini yake.

Tanganyika ilipopata uhuru mwaka 1961, Mwalimu Julius Nyerere alikuwa Waziri Mkuu na kiongozi wa serikali. Mkuu wa nchi alikuwa Malkia Elizabeth wa Uingereza.
Januari 22, 1962 Nyerere alijiuzulu wadhifa huo na Rashidi Kawawa kuchukua nafasi yake. Mabadiliko ya katiba ikaifanya Tanganyika kuwa Jamuhuri Desemba 9,1962 na Nyerere kuwa Rais. Malkia wa Uingereza akakoma kuwa mkuu wa nchi ya Tanganyika.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...