Skip to main content

Mwezi Bandia: China inaweza kuangaza mawingu usiku?

Muonekano wa mwezi kutoka kwa kitoka kwa kituo cha angani mjini Chengdu, ChinaKampuni moja ya Uchina imetangaza mpango wake wa kubuni ''mwezi bandia" utakaoangaza miji usiku.
Kwa mujibu wa gazeti la kitaifa la People's Daily, maafisa katika taasisi ya kibinafsi ya masuala ya anga za juu iliyoko mjini Chengdu inataka kuzindua "kituo cha satellite kitakachoangaza" ulimwengu.
Mradi huo unatarajiwa kuzindiluwa ifikapo mwaka 2020, ambayo pia itakua na mwangaza wa haliya juu utakaochukua nafasi ya taa za barabarani.
Mpango huo umevutia hisia mbali mbali kutoka kwa wanasayansi ambao wanahoji uwezekeno wa kufikiwa kwa mpango huo huku wengine wakiukejeli.

Tunafahamu nini kuhusiana na mradi huu?
Hakuna mengi yaliyoangaaziwa kuhusiana na mradi wenyewe - taarifa zilizotolewa kwa umma pia zinakinzana.
Gazeti la People's Daily iliangzaia mradi huo kwa mara ya kwanza wiki iliyopita.
Gazeti hilo lilimnukuu mwenyekiti wa Taasisi ya mambo ya anga za mbali, Wu Chunfeng aliyegusia mpango huo.
Bwana Wu amesema mradi huo mpya umekua ukifanyiwa majaribio kwa miaka kadhaa sasa na kwamba teknolojia hiyo iko tayari kuzinduliwa ifikapo mwaka 2020.
Haijabainika ikiwa mradi huo umeidhinishwa rasmi na serikali.

Mwezi bandia utafanya vipi kazi?
Kwa mujibu wa gazeti la kitaifa la Uchina mwezi huo utafanya kazi kama kioo ambayo itakua ikielekeza mwangaza wa jua duniani
Utakua unazunguka karibu kilo mita 500- sawa na urefu wa kituo cha kimataifa cha angani.
Mzunguko wa mwezi duniani unakadirika kuwa kilo mita 380,000.

Ripoti hiyo haijatoa maelezo yoyote kuhusu muonekano wa mwezi huo bandia.
Bwana Wu amesema utakua ukileta mwangaza wa jua katika eneo 10km na 80km na utakua na unaangaza mara nane zaidi ya mwezi wa ukweli.
Wu anasema mwangaza wa mwezi huo bandia utadhibitiwa.
Tayari kuna uchafuzi wa mazingira unaotokana na mwangaza mjini Chengdu
Tayari kuna uchafuzi wa mazingira unaotokana na mwangaza mjini Chengdu
 Lakini... kwanini?
Maafisa wa taasisi ya Chengdu wanasema mwangaza huo utadhibitiwa ili kupunguza gharama.
Pia wanasema mwangaza wa mwezi bandia huenda ikawa gharama nafuu kuliko malipo ya taa za barabarani.
Dr Matteo Ceriotti, mhadhiri wa somo la uhandisi wa angaa za mbali katika chuo kikuu cha Glasgow, ameimbia BBC "Nadhani huu ni mfano wa uwekezaji,"
"Umeme unaotumika usiku ni ghali mno kwa hivyo kukipatikana mwangaza mbadala kwa miaka 15 utachangia pakubwa kuimarisha uchumi."

Lakini hilo linawezekana?
Kisayansi kuna uwezekani asema Dr Ceriotti.
Hata hivyo ili kufikia lengo lake , huo mwezi bandia lazima uwe unazunguka maisha jua ya Chengdu - katika eneo ambalo ni dogo ukilinganisha na mduara wa dunia kutoka angani.

Mradi huu utakua na athari gani kwa mazingira?
Watumiaji wa mitandao wa kijamii nchini Uchina wanamasha.
Baadhi yao wanasema tayari kuna uchafuzi wa mazingira unaotokana na mwangaza katika eneo la Chengdu na miji mingine ya China.
Wengine wanasema mwakaza huo bandia utakua na athari kwa viumbe wengine wadogo dunian.

John Barentine, mkurugenzi wa Sera ya Umma katika Chama cha Kimataifa cha Anga za giza , ameiambia jarida la habari la Forbes.
"Mwezi utaongeza mwangaza wa wakati wa usiku katika jiji ambalo tayari linakabiliwa na mwanga mkali, kwa hivyo hakuna haja ya kuwaongezea matatizo zaidi wakazi wa Chengdu,"
Dr Ceriotti pia amaiambia BBC kuwa endapo mwangaza utakua mkali zaidi huenda "ukaathiri mfumo wa usiku wa maumbile ya dunia haliambayo pia huenda ikawa na athari kwa wanyama".
Pia amesema ikiwa mwangaza huo utakua mdogo hautakua na maana yoyote.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...