Skip to main content

Mbwana Ally Samatta: Nyota wa Tanzania amfunga kipa wa Liverpool aliyekumbwa na mkosi Europa League Besiktas v KRC Genk

SamattaNahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Ally Samatta aliendelea kutikisa ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League, kwa kufungia klabu yake mabao mawili katika mechi iliyochezwa Alhamisi.
Aliisaidia klabu yake ya KRC Genk kuwalaza Besiktas wa Uturuki kwa mabao 4-2.
Katika mechi hiyo, langoni alikuwa kipa wa Liverool Loris Karius ambaye anakumbukwa kwa kufanya makosa makubwa na kuchangia Liverpool kushindwa kwenye fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mwezi Mei mwaka huu.
Samatta alifunga bao la kwanza dakika ya 23 na kisha akaongeza la pili dakika ya 70 baada ya kupokea mpira kutoka kwa Joakim Maehle nyakati zote mbili.
Mabao yote mawili aliyafunga kwa mguu wake wa kulia.
Besiktas walikomboa bao moja dakika ya 74 kupitia Vagner Loveawazisha dakika ya 74, lakini Genk wakaongeza mabao mengine mawili kupitia Dieumerci Ndongala (81') na Jakub Piotrowski (83).
Vagner Love alikombolea Besiktas bao jingine dakika ya 86 lakini hawakuwa na muda na mechi ikamalizika 4-2.
Samatta alikuwa amepiga krosi ambayo ilizalisha bao lililofungwa na Piotrowski. Aliondolewa uwanjani dakika ya 87 na nafasi yake akaingia Zinho Gano.
Haki miliki ya picha Getty Images
Sasa, nyota huyo wa Tanzania amefunga mabao matatu katika hatua ya makundi Europa League, ingawa alikuwa amefunga mengine matano mechi za muondoano za kufuzu za kabla ya hatua ya makundi.
Alifunga bao moja dhidi ya Malmo FF 20 Septemba, lakini hakufunga Sarpsborg 08 mnamo 4 Oktoba.
Katika mechi za kufuzu Europa League msimu huu, alifunga mabao mawili dhidi ya Lech Poznan, bao moja kila mechi.
Mnamo 23 Agosti 2018 Samatta, alifunga 'hat-trick' dhidi ya Brøndby IF katika Europa League kwenye mechi ambayo walishinda 5-2, na baadaye mechi ya marudiano akawafunga bao moja.
Taarifa kutoka Uingereza siku za hivi karibuni zimedokeza kwamba anatafutwa na klabu za West Ham United, Everton na Burnley kutokana na ustadi wake msimu huu katika kufunga mabao.
Haki miliki ya picha Getty Images
Samatta, mwenye kimo cha futi 5 inchi 11, amefunga mabao manane sasa Europa League msimu huu.

Masaibu ya Karius

Mjerumani huyo mwenye miaka 25 analaumiwa kwa kuwasaidia Real Madrid kushinda 3-1 kwenye fainali hiyo iliyochezewa mjini Kiev, Ukraine.
Mjerumani huyo alimpa mshambuliaji wa Real Madrid Karim Benzema bao rahisi la kwanza mjini Kiev.
Baadaye, alimruhusu Gareth Bale kufunga bao la tatu la Real kutoka mbali alipojaribu kuzuia kombora lake lakini likapita mikono yake na kutumbukia wavuni.
Haki miliki ya picha Getty Images
Image caption Loris Karius akiliwazwa
Hilo liliwawezesha Real kushinda taji la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya tatu mtawalia.
Karius alitokwa na machozi baada ya kipenga cha mwisho kupulizwa huku akionekana mwenye masikitiko makubwa.
Baadaye aliwaomba radhi wachezaji wenzake, wakufunzi na mashabiki.
Baadaye ilidaiwa kwamba huenda alikuwa anauguza jeraha la ubongo kutokana na mkitisiko wa ubongo.
Kabla yake kufanya kosa lililozalisha goli la kwanza, Karius aligongana na beki wa Uhispania Sergio Ramos.
Wakati wa kujiandaa kwa msimu mpya, Karius, 25, alidaiwa kusababisha bao la tatu la Borussia Dortmund katika mechi ambayo Liverpool walilazwa 3-1.
Kipa huyo alielekeza mkwaju kutoka kwa Christian Pulisic wa Dortmund kwenye njia ya Bruun Larsen aliyefunga bao lao la ushindi.
Alifanya kosa hilo siku chache baada yake kudaiwa kufanya kosa jingine mapema mwezi Julai mechi ya kirafiki dhidi ya Tranmere.
Alishindwa kudhibiti vyema mpira wa frikiki aliokuwa ameudaka na kuwawezesha wenyeji kufunga wakati wa mechi hiyo iliyomalizika kwa ushindi wa Liverpool wa 3-2 uwanjani Prenton Park.
Liverpool walikuwa wameongoza 3-0 kufikia wakati wa mapumziko kupitia mabao ya Rafael Camacho, Sheyi Ojo na Adam Lallana, kabla ya Jonny Smith na Amadou Soukouna kuwafungia Tranmere.

Kuhamia Uturuki

Loris Karius alihamia klabu ya Besiktas mwishoni mwa mwezi Agosti kwa mkopo wa miaka miwili.
Alikuwa amewachezea Liverpool mechi 49 tangu ajiunge nao akitokea klabu ya Mainz ya Ujerumani mwaka 2016.
Besiktas walimaliza wakiwa wa nne katika Ligi Kuu ya Uturuki msimu uliopita, alama nne nyuma ya mabingwa Galatasaray.
Liverpool walimuuza baada ya kununua kipa Alisson kutoka Brazil na kumfanya kuwa kipa ghali zaidi duniani kwa wakati huo kwa uhamisho wa £66.8m (euro 72.5m).

Kuvuma kwa Samatta akiwa TP Mazembe

Samatta alijiunga na Genk akitokea TP Mazembe Januari 2016 ambapo alitia saini mkataba wa kumuweka katika klabu hiyo hadi msimu wa 2019/20.
Amesalia na miezi 20 hivi kabla ya mkataba wake kumalizika.

Comments

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...