Skip to main content

Majambazi wa Ubelgiji waliambiwa warudi tena - na waliporudi wakatiwa mbaroni

Picha ya CCTV ikionyesha watu wanaodaiwa kuwa wezi waliojihami kwa visu wakizungumza na mwenye dukaGenge la majambazi liliingia katika duka moja kwa nia ya kutaka kuiba.
Mwenye duka akawaambia warudi tena baadaye atakapokua na pesa zaidi, na majambazi hao wakaitikia mwito...
Ni tukio ambalo unaweza ukalichukulia kama mzaha, lakini kwa mwenye duka mbelgiji anayeendesha biashara ya kuuza sigara mtandaoni ni tukio la kweli na la kuogofya.
Watu sita waliingia katika duka la Didier viungani mwa mji wa Charleroi wakiwa na mpango wa kumuibia.
Mfanyibiashara huyo aliwaambia wezi hao kurejea dukani hapo mwisho wa siku, wakati atakapokua na pesa nyingi za kuwapatia.
Bila kusita watu hao walirejia kama walivyoagizwa na mwenyeduka badala ya kuwapatia pesa alivyowaahidi wakakamatwa na polisi.
Akizungumza na BBC alisema "Ni tukio la kuchekesha,". " Wamepewa jina la majambazi wajinga zaidi nchini Ubelgiji."
Mwenye duka huyo anasema alitumia muda wa dakika 14 akijaribu kujenga uhusiano mzuri na wezi hao.
Didier anasema kuwa alibishana nao kidogo," "Sikuwapatia kitu chochote, lakini nikawaambia wakirudi baadaye nitakua na kama uero 2,000 ama 3,000."
Wezi hao walikubaliana na mwenye duka na kuondoka.
"Nilipowaarifu maafisa wa polisi, hawakuamini wezi hao wangelirudi."
Lakini ilipofika saa kumi na moja unusu jioni walirudi.
Didier anasema kuwa alimuona mmoja wa wezi hao mlangoni akamwambia bado hajakamilisha biashara ya siku.
Wanaume hao waliporejea saa kumi na mbili na nusu jioni, wakakamtwa na maafisa wa polisi ambao walikua wamejificha ndani ya duka hilo tayari kuwakamata.
Wanaume watano walikamatwa miongoni mwao kijana mdogo

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...