Skip to main content

Mwanafunzi ashtakiwa baada ya kumtishia mwalimu silaha bandia

Waziri wa elimu wa Ufaransa Jean-Michel BlanquerMwanafunzi mmoja ameshtakiwa kwa kosa la kusababisha mtafaruku baada ya picha ya video ikimuonyesha akimtisha mwalimu wake silaha bandia, mjini Paris, waendesha mashtaka wameeleza.
Tukio hilo lilirekodiwa na kuwekwa mitandaoni na mmoja wa wanafunzi wenzake
Mvulana huyo mwenye miaka 15 alisema kuwa alifanya ''mzaha'' na kuongeza kuwa hakujua kama alikuwa akirekodiwa,vyombo vya habari nchini ufaransa vimeripoti.
Mwalimu huyo alipeleka malalamiko yake polisi siku ya Ijumaa.
Mwanafunzi huyo alikwenda polisi siku hiyohiyo akiwa kaongozana na baba yake.
Katika video, alionekana akimnyooshea silaha bandia mwalimu wake, aliyekuwa amekaa kwenye dawati.Alimpigia kelele akimtaka amuorodheshe kuwa alikuwa darasani.
Mwalimu aliendelea kufanya kazi kwenye Kompyuta yake huku akizungumza na wanafunzi.
Gazeti moja jijini Paris limeripoti kuwa mwanafunzi huyo alipandwa na ghadhabu kwa kuwa aliandikwa kwenye orodha kwamba hakuwa darasani baada ya kufika darasani katika shule ya Edouard-Branly akiwa amechelewa.
Tukio hilo limekemewa vikali na waziri wa mambo ya ndani wa Ufaransa,Christophe Castaner.
Katika ukurasa wake wa Twitter, Rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron amesema tukio hilo ''halikubaliki''.
Mkutano wa kujadili namna ya kukomesha vitendo vya ghasia shuleni utafanyika viungani mwa jiji la Paris.
Didier Sablic,amekuwa mwalimu wa shule hiyo kwa miaka 25, ameliambia gazeti la Le Monde kuwa ''hajazoea matukio ya namna hii'' , alisema wanafunzi shuleni hapo hufundishwa ''namna ya kuwasiliana na nidham

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...