Skip to main content

Kulala bila nguo kuna hatari zozote?

usingiziHaki miliki ya picha
Kila mtu huwa ana namna yake ya kulala ambayo anajiona kuwa yuko huru
Takwimu zinaonesha kwamba idadi kubwa ya vijana, na hasa Ulaya, huwa hawavai nguo ya aina yoyote ile wanapolala.
Je, kuna madhara au manufaa? Unafaa kulala bila nguo?
Mtaalam wa usingizi Dkt Nerina Ramlakhan ameambia BBC kwamba kuna faida ambazo mtu anaweza kuzipata akivaa nguo za kulalia wakati anapolala.
"Kila mtu ana upekee wake na kila mtu ana namna yake ya kulala ambayo anaona huwa inampa uhuru au raha. Kuna baadhi ya watu hawapendi kulala bila nguo huku wengine huwa hawajali kabisa," Dkt Ramlakhan.
Anaongeza kwamba kila mtu huwa anahitaji kiwango cha joto ambacho kwake kinamfanya aweze kulala vizuri, na kwa kawaida huwa chini kidogo ya kiwango cha joto mwilini.
Anashauri kuwa kama unavaa nguo wakati wa kulala au huvai ni vyema kutumia kitanda chenye godoro zuri, na vilevile vazi zuri la kulalia ni lile la nguo nyepesi.
Je, kuna ubaya wa kulala bila nguo?
Dkt. Ramlakhan anasema kwamba hawezi kufikiria sababu yoyote mbaya inayohusisha mtu kulala bila nguo… 'kama mtu unajisikia vizuri kulala bila nguo basi ni vyema kufanya hivyo'.
Ukilala bila nguo unaweza kujihisi huru zaidi.
Hata hivyo, changamoto hutokea ukiwa ugenini.
Ni vyema kuzingatia kama unaweza kuwakwaza watu wengine ambao labda umelala nao, kwa mfano iwapo utalazimika kuamka kwa dharura usiku.
Unaweza pia kuwa makini kwa kuamka mapema kabla ya watu wengine kuamka, iwapo kwa mfano umelala eneo la wazi ambapo wenyeji wako pia wanatumia.
usingiziHaki miliki ya picha
Mambo 5 yanayoweza kukufanya ulale vizuri
  1. Kupata kiamsha kinywa ndani ya nusu saa au saa moja baada ya kuamka, haswa kama unajisikia uchovu. Ni muhimu kula kitu ili kutuliza mzunguko wa damu na sukari.
  2. Punguza unywaji wa kahawa au vinywaji vingine vyenye kafeini kwa kula chakula kama mbadala wake.
  3. Kunywa maji kwa wingi; Maji katika mwili huchukua asiliia 60 hivyo ni vyema unywe lita mbili za maji kila siku. Maji ya matunda(juice) pia ni mazuri lakini sio chai au kahawa.
  4. Jitenge na matumizi ya simu wakati wote mchana, pumzisha macho kiasi. Usilale na simu yako karibu au kuiwasha simu kuwa ndio kitu cha kwanza unafanya asubuhi.
  5. Lala mapema mara tatu au nne kwa wiki. Si lazima ulale moja kwa moja, unaweza kusoma kitabu au kufikiria jinsi siku yako ilivyokuwa.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...

Je unayafahamu maajabu ya Ziwa Ngosi Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika inayozungukwa na vivutio vingi vya utalii na vingine inawezekana hata havitambuliwi na wenyeji. Ziwa Ngosi yawezekana kuwa ni miongoni mwa vivutio hivyo. Ziwa hili ambalo ni la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya ziwa lingine la kreta lililopo Ethiopia linaakisi muonekano wa bara la Afrika katika upande wa kusini, magharibi, kaskazini na mashariki pamoja na visiwa vyake vya Unguja na Pemba.