Skip to main content

Vijana wanavyokabiliana na 'uhaba' wa kondomu Zanzibar

Kondomu
Mashirika ya kijamii yamekuwa mstari wa mbele katika kampeni mbalimbali za kuhamasisha matumizi ya mipira ya kondom ili kuzua maambukiza ya magonjwa ya zinaa.
Lakini katika baadhi ya maeneo visiwani Zanzibar matumizi ya kondomu si jambo la kawaida.
Kondomu haiuzwi katika maduka ya kawaida, jambo ambao limekua likiwaumisha vichwa wanaharakati wa chama cha watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi visiwani humo.
Kwa mujibu wa Wizara ya afya Zanzibar, maambukizi ya virusi vya Ukimwi yapo chini ya 1% lakini kwa upande wa makundi hatarishi kama vile watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi na pamoja na wanawake wanaofanya biashara ya ngono bado maambukizi ni makubwa.

BBC imebaini kuwa changamoto kuu ni upatikanaji wa mipira ya kondomu hasa katika maduka ya kawaida.
''Ishawahi kunitokea'' ,anasema mmoja wa wanawake wanaofanya biashara ya ngono.
''Nataka kondomu lakini sehemu ya kupata hamna, inabidi kama sehemu ya kuppata hmna inabidi siku kama hiyo ndi sifanyi kazi'' anasema mwanamke huyo.
Aliongeza kuwa visiwani Zanzibar ukienda kuulizia kundomu watu wanakushangaa sana.
Aliwahi kununua kondomu katika duka la kawaida lakini alipata jibu aambalo lilimuacha na maswali mengi
''Eti wataka kondomu? mimi siuuzi kondomu hapa, wewe dada unanivunjia heshima'', alisema mwanamke huyo.
Hata hivyo kuna badhi ya wakaazi ambao wanasema siku hizi mambo yamebadilika sio kama ilivyokuwa zamani.
Zanzibar
 Jamii ya Zanzibar ni ya kihafidhina ambapo matumizi ya kondomu hayakubaliki

''Sasa hivi kondomu zipo kwa hivyo mtu huwezi kufanya mapenzi kiholela bila ya kutumia kondomu'' mwanamake mwingine aliiambia BBC.
Baadhi ya vijana wanofanya kazi na na kujitolea katika chama cha watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi wamewahi kukumbwa na adha ya upatikanaji wa kondomu.
Wanasema jambo hilo ni tatizo kubwa zaidi kwa vijana vijana wa kawaida.
Kwa kiasi kikubwa jamii ya Wazanzibari wanaona matimizi ya kondomu ni sehemu ya uchochezi wa ngono.
Hata hivyo Tume ya Ukimwi visiwani humo inapania kuja na mkakati ambao utasaidia kutatua suala hilo.
''Kondomu kwetu Zanzibar ni suala ambalo kidogo ni nyeti'' anasema afisa wa Tume hiyo, Siaba Saadati.
Anasema kwenye jamii viwango vya maambukizi ni madogo lakini katika makundi maalum ni makubwa.
''Hapa katikati lazima lazima tuje na mbinu ya kuwakinga watu'' aliongeza Bw. Saadati.
Hata hivyo amekiri kuwa ipo haja ya wao kuja na mkakati ambao utalingana na hali halisi ya mila na desturi ya kizanzibari.
Mbali na kuwa maambukizi ya Ukimwi kuwa chini visiwani Zanzibar bado wadau wa masuala ya afya wanasisitiza juu ya upatikanaji wa uhakika wa kondomu katika maduka na sehemu za wazi.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...