Skip to main content

Itambue miji yenye gharama kubwa na gharama za chini kuishi duniani

Eiffel towerHaki miliki ya pich IMAGES
Paris ndio mji ulio na gharama kubwa zaidi duniani, ukiandamana na Hong Kong na Singapore.
Ni mara ya kwanza miji mitatu imekuwa katika nafasi sawa juu katika historia ya miaka 30 ya utafiti wa kila mwaka wa uchumi - Economist Intelligence Unit, inayolinganisha gharama katika miji 133 duniani.
Mji mkuu wa Ufaransa - ulio katika nafasi ya pili kwa gharam kubwa ya maisha mwaka jana - ndio nchi ya pekee ya Ulaya iliopo katika nafasi ya juu mwaka huu.
Utafiti huo umelinganisha bei za bidhaa za kawaida kama mkate katika miji 133.
Alafu inafuatilia iwapo bei hizo zimepanda au zimeshuka kwa kuzilinganisha na gharama ya maisha katika mji wa New York, Marekani.

Mithilisho

Mhariri wa ripoti hiyo Roxana Slavcheva amesema Paris umekuwa mojwapo ya miji kumi iliyo na gharama kubwa kuishi tangu 2003.
"Ni pombe tu, usafiri na tumbaku ulio na gharama nafuu ikilinganihswa na mataifa mengine ya Ulaya," amesema.
Kiwango cha gharama kwa mwanamke kukatwa nywele, kwa mfano inagharimu $119.04 mjini Paris, $73.97 mjini Zurich na $53.46 mjini Osaka nchini Japan.

Miji 10 yenye gharama kubwa duniani
1. Singapore (Singapore)
1. Paris (Ufaransa)
1. Hong Kong (China)
4. Zurich (Uswizi)
5. Geneva (uswizi)
5. Osaka (Japan)
7. Seoul (Korea Kusini)
7. Copenhagen (Denmark)
7. New York(Marekani)
10. Tel Aviv (Israeli)
10. Los Angeles (Marekani)

Barber in CaracasHaki miliki ya pichIMAGES
Mfumko wa bei na kutetelekea kwa sarafu kumesaidia msukumo wa mageuzi katika orodha ya mwaka huu huku matiafa kama Argentina, Brazil, Uturuki na Venezuela zikishuhudia kupungua kwa ukubwa gharama ya maisha .
Caracas huko Venezuela, ambako mfumko wa bei ulikaribia 1,000,000% mwaka jana na kuilazimu serikali kuidhinihsa sarafu mpya, ulioorodheshwa mji wenye gharama ndogo zaidi duniani mwaka huu.
Damascus nchini Syria iliorodheshwa mji wa pili wenye gharama ndogo zaiid duniani.
Utafiti huo wa Economist Intelligence Unit umeeleza kwamba "baadhi ya maeneo" gharama ya kuishi inapungua kutokana na athari za mtikisiko wa kisiasa au kiuchumi.

Miji 10 yenye gharama ya chini duniani

1. Caracas (Venezuela)
2. Damascus (Syria)
3. Tashkent (Uzbekistan)
4. Almaty (Kazakhstan)
5. Bangalore (India)
6. Karachi (Pakistan)
6. Lagos (Nigeria)
7. Buenos Aires (Argentina)
7. Chennai (India)
8. New Delhi (India)

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...