Skip to main content

Je Familia ya Kardashian imetoa wapi mamilioni ya dola?

Kris Jenner, Khloe Kardashian, Kendall Jenner, Kourtney Kardashian, Kim Kardashian West, North West, Caitlyn Jenner and Kylie JennerHaki miliki ya pich IMAGES


Image captionKutoka kushoto, Kris Jenner, Khloe Kardashian, Kendall Jenner, Kourtney Kardashian, Kim Kardashian West, North West, Caitlyn Jenner na Kylie Jenner

Kipindi cha Televisheni kinachoonesha maihsa ya uhalisi 'Keeping up with the Kardashians' kimeanza upya kwa msimu wa 16, kumaanisha mvutano na malumbano ya familia hiyo yanaywekwa parwanja kwa mara nyingine.
Kipindi hicho kimekuwa kikipeperushwa kwa muda unaozidi muongo mmoja sasa, huku utajiri wa familia huo ukikuwa kwa kadri ya miaka ya kipindi hicho.
Kylie Jenner - ambaye wakati kipindi hicho ha TV kilipoanza alikuwa na miaka 9 - sasa ana miaka 21 na ni bilionea.
Akiwa na utajiri unaokadiriwa $1bn (£760m), kwa mujibu wa jarida la Forbes, mwanadada huyo mmiliki wa kampuni ya vipodozi ndiye aliye tajiri zaidi kati ya wanfamailia nzima ya Kardashian clan, inayoongozwa na kusimamiwa na mama Kris Jenner.
Hatahivyo, ndugu zake wengine pia sio kwamba hawajiwezi.
Kim Kardashian West ni tajiri mwenye mamilioni ya dola kutokana na kampuni yake pia ya vipodozi na manukato; Kendall Jenner ni mwanamitindo wa kimataifa; Khloe Kardashian ana kampuni ya kuuza suruali aina ya jeans na dada mkubwa kabisa Kourtney Kardashian amefaidika kutokana na kushirikishwa katika matangazo ya biashara na kampuni za kutengeneza nguo.
Kwa kuchanganya kazi na maisha binfasi na utajiri unaotokana na uwepo wao katika mitandao ya kijamii umedhihirika kuwnaa faida kubwa kwao.


Kylie JennerHaki miliki ya pichaES
Image captionKylie Jenner ametajirika kutokana na kampuni yake ya vipodozi

Alexander McKelvie, mhadhiri kuhusu masuala ya ujasiriamali kutoka chuo kikuu cha Syracuse anamaini pia kipindi chao kimeandikwa vizuri sana.
"Unapokikagua kipindi hicho unaweza kufikiria ni matukio ya papo kwa hapo," amesema.
"lakini huenda tamthilia imeandikwa na kupangwa vizuri kwa ujumbe wa kuvutia kuhusu wasimamizi wa kipindi na familia yenyewe wanachotaka kijulikane kuwahusu."

Familia ya Kardashian imetoa wapi mamilioni ya dola?

Msimu mpya wa kipindi cha Keeping up with the Kardashians kinalenga kuangazia "kashfa" inayowahusu Khloe Kardashian, aliyekuwa mpenzi wake Tristan Thompson na anayeonekana kuwa 'mchepuko' rafiki wa dhati wa Kylie Jenner, Jordyn Woods.
Katika kipindi hicho, Khloe analalamika: "Inaudhi kwamba limekuwa jambolinalojulikana na umma. Sio kwamba ni makala ya Televisheni, haya ni maisha yangu binafsi."
Kwa wakati ambapo kashfa hii ilipofichuka, bei ya rangi ya mdomo 'Jordy Lip Kit', bidhaa iliyotokana na ushirikiano wa Kylie na Jordyn, ilishushwa bei kwa 50%.
Iliuzika mpaka ikamalizika
Ni wazi kwamba kashfa hiyo iligueza hesabu.


Kourtney Kardashian and Kim Kardashian WestHaki miliki ya pichERS
Image captionKourtney Kardashian,na Kim Kardashian West, wameanzisha blogu

Wakati Kylie alipozindua rangi za mdomo mnamo Novemba 2015, alifanikiwa kuwauzia mamilioni ya mashabiki moja kwa moja kupitia mtandao wa kijamii iliomaanisha kwamba alifanikiwa kukwepa gharama ya kunadi bidhaa katika soko na alipata faida ya kujua hisia za watumiaji moja kwa moja iwapo wameipenda au hawakuipenda bidhaa hiyo.
Je familia hii inatengeneza pesa daima?
Baadhi ya mikataba ambayo familia hiyo imefikia katika miaka ya kwanza ya ufahari wao hususan kwa kuwahusisha ndugu zake wakubwa Kourtney, Kim na Khloe, haijakuwa rahisi au shwari.
Dada hao walikuwa sura ya kampen iya vipodozi iliyopewa jina Khroma Beauty kupiitia kibali cha makubaliano.
Lakini baada ya uzinduzi mnamo 2012, vipodozi hivyo viliondolea kutoka madukani kutokana na tuhuma za ukiukaji wa haki miliki.
Baadaye zikarudishwa kwa jina jipya la Kardashian Beauty, lakini bado waliandamwa kisheria. Ni hivi karibuni tu ambapo familia hiyo imefanikiwa kujitoa katika kesi hiyo.


Khloe Kardashian, Kylie Jenner, Kris Jenner, Kourtney Kardashian, Kim Kardashian and Kendall JennerHaki miliki ya pichS

Walizindua pia Kardashian Kard, kadi ya kuchukua bidhaa kwa akiba zilizolengwa vijana na wazazi wanaotaka kufuatilia matumizi ya watoto wao.
Iliondoshwa hatahivyo baada ya aliyekuwa mkuu wa sheria wa jimbo la Connecticut Richard Blumenthal kusema kwamba ana wasiwasi na gharama kubwa ya kadi hizo.
Na hata sasa, sio kila kitu wanachoianzisha kinafanikiwa.
Tangazo la Kendall Jenner na kampuni ya kinywaji Pepsi lilikabiliwa na shutuma kali na hasira dhidi ya tangazo hilo ambalo baadhi waliliona kupuuzia uzito wa mauaji ya watu weusi Marekani kupitia vuguvugu la Black Lives Matter movement.
Pepsi iliondoa tangazo hilo siku moja baada ya kupeperushwa.
Na si hayo tu, familia hiyo imeshutumiwa pakubwa kwa kupokea fedha katika kuendekeza na kuhimiza matumizi ya bidhaa za kupunguza uzito wa mwili.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...