Skip to main content

Vimbunga vilivyopewa majina duniani(Kimbunga Kenneth, Matthew, Katrina).



Kimbunga HermineHaki miliki ya picha

Umewahi kusikia vimbunga vikiwa na majina ya kushangaza, kilichoitwa Idai kilichosababisha uharibifu mkubwa katika baadhi ya maeneo nchini Msumbiji, Malawi na Zimbabwe mwezi uliopita Machi katika kile ambacho Umoja wa mataifa unasema huenda ni janga baya zaidi la hali ya hewa kuwahi kushuhudiwa kusini mwa Afrika.
Matthew ambacho kilikumba maeneo ya Haiti, Jamaica, Jamhuri ya Dominika, Bahamas na baadhi ya majimbo ya Marekani mwezi Oktoba mwaka 2016.
Mwezi uliotangulia kulikuwa na kimbunga kingine kilichojulikana kama Hermine ambacho kilisababisha uharibifu mkubwa jimbo la Florida.
Lakini kinachokumbukwa sana ni kile kwa jina Katrina ambacho kiliathiri sana majimbo ya Louisiana, Mississippi na Alabama nchini Marekani.

Je, vimbunga hivi hupewa vipi majina?



Uharibifu wa kimbunga Hermine
Haki miliki ya pichTERS


Vimbunga vinavyopewa majina
Vimbunga katika maeneo ya bahari ya Atlantiki, maeneo ya Caribbean na Ghuba ya Mexico hupewa majina ya Shirika la Utabiri wa Hali ya Hewa Duniani (WMO) ambalo lina makao yake makuu nchini Uswizi.
Zamani, ni majina ya kike pekee yaliyotumiwa lakini kuanzia 1979, majina ya kiume yalianza kutumiwa.
Huwa kuna makundi sita ya majina ambayo hutumiwa kwa mzunguko.
Hii ina maana kwamba majina yaliyotumiwa kwenye vimbunga mwaka hu hayatatumiwa tena hadi 2022.
Majina kwenye orodha hii yanaweza kubadilishwa na WMO.
Orodha hii ilianza kutumiwa mwaka 1979. Kabla ya hapo, jina la kimbunga Fern lilibadilishwa mwaka 1966 na badala yake kukatumiwa Frieda. Hakuna sababu iliyotolewa.

Majina yanavyoacha kutumiwa

Haki miliki ya picMajina yanavyoacha kutuBaadhi ya majina huacha kutumiwa, sana kunapotokea uharibifu mkubwa au hasara kubwa hivi kwamba kutumia tena jina hilo kutafufua kumbukumbu zenye uchungu.

Mfano ni kimbunga Katrina kilichoua watu 2,000 mwaka 2005 na kusababisha uharibifu mkubwa Marekani.
Kimbunga hicho kiliwaacha watu milioni moja bila makao. Mji wa New Orleans, Louisiana uliathirika sana.
Katika WMO kuna kundi la wataalamu liitwalo Kamati ya Vimbunga vya Tropiki ambalo hukutana kila mwaka.
Kundi hilo ndilo huamua ni majina yapi yatatumika tena na ni yapi yataacha kutumiwa.

Majina yaliyoacha kutumiwa

Kando na Katrina, kuna majina mengine ambayo yameacha kutumiwa. Mitch, kutokana na kimbunga cha mwaka 1998 kilichoua watu 11,000 Honduras na Nicaragua, halitumiwi tena. Kimbunga hicho ndicho kibaya zaidi kukumba maeneo ya Magharibi mwa dunia katika kipindi cha miongo miwili iliyopita.






Tegucigalpa nchini HondurasHaki miliki ya picha

Kimbunga Sandy cha mwaka 2012 na Kimbunga Irene 2011 pia vilisababisha uharibifu mkubwa. Majina hayo hayatumiwi tena.
Kimbunga hatari zaidi kuwahi kukumba Marekani kilitokea 1780, ambapo kiliua watu 22,000 maeneo yaMartinique, Barbados na St Eustatius.
Wakati huo majina hayakuwa yameanza kutumiwa kurejelea vimbunga.

Majina yaliyoacha kutumiwa tangu 1954.



Retired hurricane namesHaki miliki ya pichaNATIONAL HURRICANE CENTER

Majina maeneo mengine duniani

Katika maeneo mengine duniani, huwa kuna utaratibu tofauti wa kuvipa majina vimbunga.
Lakini majina yote hupitia kwa WMO.
Kwa mfano, maeneo ya Kaskazini Magharibi mwa Pasifiki na Bahari ya China Kusini, kuna jedwali la majina ambalo kila taifa linaloathirika huchangia.
Baada ya kimbunga kutokea, kimbunga kinachofuata hupewa jina linalofuata.
Kwa mfano, kimbunga cha kwanza huitwa Damrey (kimbunga cha kwanza Cambondia) na kitakachofuata kinafaa kuitwa Kaikui (jina la kwanza China).
Kimbunga cha sasa maeneo hayo ni Chaba (jina la nafasi ya nne Thailand).
Kilichotokea majuzi kiliitwa Megi na ambacho kiliathiri maeneo ya China na Taiwan. Jina hilo ni la nafasi ya nne chini ya majina ya Korea Kusini.

List of Western North Pacific and South China Sea storm namesHaki miliki ya pichaWORLD METEOROLOGICAL ORGANISATION

Majina ya vimbunga na tufani yalianza kutumiwa Uingereza na Ireland, kwa majaribio.
Kuna jina kwa kila alfabeti, isipokuwa Q, U, X, Y na Z, ambao ndio utaratibu unaotumiwa kuvipa majina vimbunga Atlantiki Kaskazini.

Comments

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...