Skip to main content

Hoteli ya DusitD2 Nairobi: Washukiwa watano wa shambulio la Dusit wawasilishwa mahakamani wakificha nyuso zao



Mmoja wa washambuliaji wa Hoteli ya FDusit alyeuawa na vikosi vya usalama vya Kenya
Washukiwa watano wanaohusishwa na shambulio la Jumanne la hoteli ya Dusit mjini Nairobi wamewasilishwa mahakamani .
Watano hao ni pamoja na raia mmoja wa Canada.
Mahakama iliruhusu upande wa mashtaka kuwaweka rumande kwa siku 30 huku uchunguzi ukiendelea.
Takriban watu 21 waliuawa wakati wapiganaji walipovamia hoteli ya DusitD2 .
Wanaume wanne walisimamishwa kizimbani katika mahakama kuu jijini Nairobi huku wakificha nyuso zao.
Ni washukiwa wa kwanza kuwasilishwa mahakamani wakihusishwa na shambulio hilo baya katika hoteli ya DusitD2 . Lakini hawakusomewa mashtaka yao.
Mkurugenzi wa mashtaka ametaka kupewa muda zaidi ili kufanya uchunguzi alioutaja kuwa mgumu na wa kimataifa.
Washukiwa wanne ni raia wa Kenya huku wa tano akiwa raia wa Canada mwenye mizizi ya Kisomali.,
Mapema maafisa wa polisi waliambia BBC waliwakamata watu saba.
Mtu mmoja ambaye alionekana na washukiwa hao kabla ya shambulio anaaminika kuwa miongoni mwa wale waliozuiliwa lakini hakuwasilishwa mahakamani mapema leo.

Fahamu kuhusu washukiwa waliokamatwa

Washambuliaji wa hoteli ya DusitD2
Watu tisa wametiwa mbaroni kuhusiana na shambulio dhidi ya hoteli ya kifahari mjini Nairobi, Kenya ambapo watu 21 waliuawa.
Washambuliaji wote watano waliyovamia hoteli ya DusitD2 na majengo yaliyokuwa karibu na hapo waliuawa, maafisa walisema huku msako wa kuwatafuta wale waliowasaidia kupanga shambulio hiloukiendelea.
Kundi la al-Shabab lenye makao yake nchini Somalia lemekiri kuhusika na shambulio hili la siku ya Jumanne.
Shirika la Msalaba Mwekundu limesema kuwa watu wote waliokuwa hawajulikani waliko wamepatikana.
Kumekuwa na taarifa za kukinzana kuhusu mwanamke anayetuhumiwa kuwa mke wa mojawapo ya washukiwa wa shambulio hilo, anayearifiwa alikamatwa Kiambu kaskazini mwa mji mkuu wa Nairobi.
Polisi inasema haiwezi kuthibitisha au kupinga kwamba kuna aliyekamatwa.
'' Hatutaweza kuzungumzia upelelezi wakati huu, kwa mfano tukizungumza kuhusu Kerubo wale waliokuwa karibu na yeye watasikia tumetangaza kuwa tunamtafuta,tunafanya nini...watatoroka'', alisema msemaji wa polisi Charlse Owino.
Aliongeza kuwa cha msingi ni kuhakikisha kuwa wale wote waliyohusika na kupanga na kutekeleza shambulia hilo wanakamatwa.

Tunafahamu nini kuwahusu washambuliaji?

Chombo kimoja cha habari nchini Kenya kinaripoti kuwa anayetuhumiwa kuwa mke wa mmoja wa washukiwa wa shambulio hilo amekamtwa katika eneo la Kiambu, kaskazini mwa mji mkuu wa Nairobi.
Polisi pia inasema kuwa imemtambua Ali Salim Gichunge, anaefahamika kwa jina lingine kama Farouk, kupitia gari lililotumika kufanya shambulio hilo.
Polisi wanashika doria nje ya nyumba ya mmoja wa washukiwa katika kaunti ya KiambuHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPolisi wanashika doria nje ya nyumba ya mmoja wa washukiwa katika kaunti ya Kiambu
Majirani wameliambia gazeti la The Standard kwamba Ali Salim Gichunge na mke wake walihamia mtaa huo mwezi Oktoba mwaka jana.
Wanasema kuwa wawili hao walikua wasiri sana na kwamba walitangaza kuuza vyombo vyao kabla ya shambulio hilo wakisema ''wanahama Nairobi wiki hii".
Magari yashika moto wakati wa shambulio la Hoteli ya kifahari ya Dusit D2 iliopo katika eneo la Riverside jijini Nairobi.
Image captionMagari yashika moto wakati wa shambulio la Hoteli ya kifahari ya Dusit D2 iliopo katika eneo la Riverside jijini Nairobi.
Al-Shabab walitoa taarifa kuhusiana na shambulio hilo wakisema kuwa ''tunalipiza kisasi uamuzi tata wa rais wa Marekani Donald Trump kutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel''
Msemaji wa baraza la usalama katika ikulu ya White House amejibu taarifa hiyo akisema: "Shambulio hili ni ishara inayotilia mkazo azma ya Marekani ya kukabiliana na ugaidi."
Je wavamizi walitekeleza vipi shambulio hilo?
Shambulio hilo lilianza mwendo wa saa tisa jioni siku ya Jumanne wakati wapiganaji wanne walirusha mabomu katika magari yaliokuwa yameegeshwa kabla ya kuingia ndani ambapo mmoja wao alijilipua, kulingana na maafisa wa polisiSiku ya Jumanne rais Uhuru Kenyatta alisema kuwa wanamgambo wakijihadi waliotekeleza shambulizi hilo ''waliangamizwa'' na vikosi vya usalamabaada ya saa 19.
Kufikia mwendo wa saa tano waziri wa usalama Fred Matiang'i alisema kuwa ,usalama umeimarishwa katika majengo yote yaliokuwa katika eneo hilo.
''Usalama umeimarishwa na taifa lipo salama'' , aliambia wanahabari. ''Ugaidi hautatushinda''.
Lakini saa moja baadaye ufyatulianaji wa risasi na milipuko iliripoitiwa katika eneo hilo.
Kulikuwa na ufyatulianaji mwengine mkali mwendo wa saa moja.
Maafisa wa usalama walilipekua eneo hilo na kuingia ambapo walikutana na wafanyikazi walioogopa. Alafajiri siku ya Jumatano , zaidi ya watu 100 waliokolewa.

Ramani ya Hoteli ya DusitD2 Nairobi

Ramani
Hoteli hiyo ya DusitD2 ina vyumba 101. ikiwa katika eneo la Westlands , dakika chache kutoka katikakati mwa jiji la Nairobi ina migahawa kadhaa.
Kenya imeshuhudia visa kadhaa vya mashambulizi katika siku za hivi karibuni-hususan katika maeneo yaliopo karibu na Somalia pamoja na mji mkuu wa Kenya.
Kwa jumla watu 700 waliokolewa kutoka jengo hilo, maafisa walisema.
28 kati ya hao wanauguza majeraha katika hospitali tofauti jijini Nairobi.
Baadhi ya wale waliyouawa walikua wakila chakula cha mchana katika mgahawa wa Secret Garden restaurant.
Miili mingine ilipatikana katika ghorofa ya tatu ya jengo la hoteli ya DusitD2.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...