Skip to main content

Hoteli ya DusitD2 Nairobi: Washukiwa watano wa shambulio la Dusit wawasilishwa mahakamani wakificha nyuso zao



Mmoja wa washambuliaji wa Hoteli ya FDusit alyeuawa na vikosi vya usalama vya Kenya
Washukiwa watano wanaohusishwa na shambulio la Jumanne la hoteli ya Dusit mjini Nairobi wamewasilishwa mahakamani .
Watano hao ni pamoja na raia mmoja wa Canada.
Mahakama iliruhusu upande wa mashtaka kuwaweka rumande kwa siku 30 huku uchunguzi ukiendelea.
Takriban watu 21 waliuawa wakati wapiganaji walipovamia hoteli ya DusitD2 .
Wanaume wanne walisimamishwa kizimbani katika mahakama kuu jijini Nairobi huku wakificha nyuso zao.
Ni washukiwa wa kwanza kuwasilishwa mahakamani wakihusishwa na shambulio hilo baya katika hoteli ya DusitD2 . Lakini hawakusomewa mashtaka yao.
Mkurugenzi wa mashtaka ametaka kupewa muda zaidi ili kufanya uchunguzi alioutaja kuwa mgumu na wa kimataifa.
Washukiwa wanne ni raia wa Kenya huku wa tano akiwa raia wa Canada mwenye mizizi ya Kisomali.,
Mapema maafisa wa polisi waliambia BBC waliwakamata watu saba.
Mtu mmoja ambaye alionekana na washukiwa hao kabla ya shambulio anaaminika kuwa miongoni mwa wale waliozuiliwa lakini hakuwasilishwa mahakamani mapema leo.

Fahamu kuhusu washukiwa waliokamatwa

Washambuliaji wa hoteli ya DusitD2
Watu tisa wametiwa mbaroni kuhusiana na shambulio dhidi ya hoteli ya kifahari mjini Nairobi, Kenya ambapo watu 21 waliuawa.
Washambuliaji wote watano waliyovamia hoteli ya DusitD2 na majengo yaliyokuwa karibu na hapo waliuawa, maafisa walisema huku msako wa kuwatafuta wale waliowasaidia kupanga shambulio hiloukiendelea.
Kundi la al-Shabab lenye makao yake nchini Somalia lemekiri kuhusika na shambulio hili la siku ya Jumanne.
Shirika la Msalaba Mwekundu limesema kuwa watu wote waliokuwa hawajulikani waliko wamepatikana.
Kumekuwa na taarifa za kukinzana kuhusu mwanamke anayetuhumiwa kuwa mke wa mojawapo ya washukiwa wa shambulio hilo, anayearifiwa alikamatwa Kiambu kaskazini mwa mji mkuu wa Nairobi.
Polisi inasema haiwezi kuthibitisha au kupinga kwamba kuna aliyekamatwa.
'' Hatutaweza kuzungumzia upelelezi wakati huu, kwa mfano tukizungumza kuhusu Kerubo wale waliokuwa karibu na yeye watasikia tumetangaza kuwa tunamtafuta,tunafanya nini...watatoroka'', alisema msemaji wa polisi Charlse Owino.
Aliongeza kuwa cha msingi ni kuhakikisha kuwa wale wote waliyohusika na kupanga na kutekeleza shambulia hilo wanakamatwa.

Tunafahamu nini kuwahusu washambuliaji?

Chombo kimoja cha habari nchini Kenya kinaripoti kuwa anayetuhumiwa kuwa mke wa mmoja wa washukiwa wa shambulio hilo amekamtwa katika eneo la Kiambu, kaskazini mwa mji mkuu wa Nairobi.
Polisi pia inasema kuwa imemtambua Ali Salim Gichunge, anaefahamika kwa jina lingine kama Farouk, kupitia gari lililotumika kufanya shambulio hilo.
Polisi wanashika doria nje ya nyumba ya mmoja wa washukiwa katika kaunti ya KiambuHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPolisi wanashika doria nje ya nyumba ya mmoja wa washukiwa katika kaunti ya Kiambu
Majirani wameliambia gazeti la The Standard kwamba Ali Salim Gichunge na mke wake walihamia mtaa huo mwezi Oktoba mwaka jana.
Wanasema kuwa wawili hao walikua wasiri sana na kwamba walitangaza kuuza vyombo vyao kabla ya shambulio hilo wakisema ''wanahama Nairobi wiki hii".
Magari yashika moto wakati wa shambulio la Hoteli ya kifahari ya Dusit D2 iliopo katika eneo la Riverside jijini Nairobi.
Image captionMagari yashika moto wakati wa shambulio la Hoteli ya kifahari ya Dusit D2 iliopo katika eneo la Riverside jijini Nairobi.
Al-Shabab walitoa taarifa kuhusiana na shambulio hilo wakisema kuwa ''tunalipiza kisasi uamuzi tata wa rais wa Marekani Donald Trump kutambua mji wa Jerusalem kama mji mkuu wa Israel''
Msemaji wa baraza la usalama katika ikulu ya White House amejibu taarifa hiyo akisema: "Shambulio hili ni ishara inayotilia mkazo azma ya Marekani ya kukabiliana na ugaidi."
Je wavamizi walitekeleza vipi shambulio hilo?
Shambulio hilo lilianza mwendo wa saa tisa jioni siku ya Jumanne wakati wapiganaji wanne walirusha mabomu katika magari yaliokuwa yameegeshwa kabla ya kuingia ndani ambapo mmoja wao alijilipua, kulingana na maafisa wa polisiSiku ya Jumanne rais Uhuru Kenyatta alisema kuwa wanamgambo wakijihadi waliotekeleza shambulizi hilo ''waliangamizwa'' na vikosi vya usalamabaada ya saa 19.
Kufikia mwendo wa saa tano waziri wa usalama Fred Matiang'i alisema kuwa ,usalama umeimarishwa katika majengo yote yaliokuwa katika eneo hilo.
''Usalama umeimarishwa na taifa lipo salama'' , aliambia wanahabari. ''Ugaidi hautatushinda''.
Lakini saa moja baadaye ufyatulianaji wa risasi na milipuko iliripoitiwa katika eneo hilo.
Kulikuwa na ufyatulianaji mwengine mkali mwendo wa saa moja.
Maafisa wa usalama walilipekua eneo hilo na kuingia ambapo walikutana na wafanyikazi walioogopa. Alafajiri siku ya Jumatano , zaidi ya watu 100 waliokolewa.

Ramani ya Hoteli ya DusitD2 Nairobi

Ramani
Hoteli hiyo ya DusitD2 ina vyumba 101. ikiwa katika eneo la Westlands , dakika chache kutoka katikakati mwa jiji la Nairobi ina migahawa kadhaa.
Kenya imeshuhudia visa kadhaa vya mashambulizi katika siku za hivi karibuni-hususan katika maeneo yaliopo karibu na Somalia pamoja na mji mkuu wa Kenya.
Kwa jumla watu 700 waliokolewa kutoka jengo hilo, maafisa walisema.
28 kati ya hao wanauguza majeraha katika hospitali tofauti jijini Nairobi.
Baadhi ya wale waliyouawa walikua wakila chakula cha mchana katika mgahawa wa Secret Garden restaurant.
Miili mingine ilipatikana katika ghorofa ya tatu ya jengo la hoteli ya DusitD2.

Comments

Post a Comment

Here

Popular posts from this blog

Why Ireland is VITAL to PRESIDENT Joe Biden.

  There is almost nothing that the polarised politicians in Washington can agree on these days. Bipartisan co-operation is extremely hard to find. That is with respect to an American editor Sara Smith. But there is one issue on which just about everyone sees eye to eye. And that is the value of the Good Friday Agreement (GFA), which ended 30 years of deadly violence in Northern Ireland.  The agreement itself is seen as a shining example of what can be achieved by determined diplomacy and careful negotiation.  American politicians are rightly proud of the role the US played in securing the peace. The tireless work of Senator George Mitchell as well as the intense engagement of President Bill Clinton were essential. President Biden sees the agreement as part of his own political legacy and can claim    credit   for encouraging US involvement in the peace process through the 1980s and 90s. Defending the GFA, and the relative peace it ensures, has been a h...

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian

How AI turned a Ukrainian YouTuber into a Russian “I don't want anyone to think that I ever said these horrible things in my life. Using a Ukrainian girl for a face promoting Russia. It's crazy.” Olga Loiek has seen her face appear in various videos on Chinese social media - a result of easy-to-use generative AI tools available online. “I could see my face and hear my voice. But it was all very creepy, because I saw myself saying things that I never said,” the 21-year-old, who studies at the University of Pennsylvania, told the BBC. The accounts featuring her likeness had dozens of different names like Sofia, Natasha, April, and Stacy. These “girls” were speaking in Mandarin - a language Olga had never learned. They were apparently from Russia, and talked about China-Russia friendship or advertised Russian products. “I saw like 90% of the videos were talking about China and Russia, China-Russia friendship, that we have to be strong allies, as well as advertisements for food.” O...

Mexico elects Claudia Sheinbaum as first woman president

Claudia Sheinbaum has been elected as Mexico's first woman president in an historic landslide win. Mexico's official electoral authority said preliminary results showed the 61-year-old former mayor of Mexico City winning between 58% and 60% of the vote in Sunday's election. That gives her a lead of almost 30 percentage points over her main rival, businesswoman Xóchitl Gálvez. Ms Sheinbaum will replace her mentor, outgoing President Andrés Manuel López Obrador, on 1 October. Ms Sheinbaum, a former energy scientist, has promised continuity, saying that she will continue to build on the "advances" made by Mr López Obrador. In her victory speech, she told voters: "I won't fail you." Her supporters are celebrating at the Zócalo, Mexico City's main square, waving banners reading "Claudia Sheinbaum, president". Prior to running for president, Ms Sheinbaum was mayor of Mexico City, one of the most influential political positions in the country ...