Haki miliki ya picha REUTERS Image caption Wawili hao wamesema walikwa na maisha ya furaha pamoja Mmiliki na Afisa Mtendaji Mkuu wa Amazon Jeff Bezos na mkewe MacKenzie wanatarajiwa kupeana talaka baada ya miaka 25 ya ndoa. Wawili hao wametoa taarifa ya pamoja kuhusu suala hilo kupitia mtandao wa Twitter siku ya Jumatano. "Baada ya kipindi kirefu cha mapenzi na kujaribu kutengana, tumeamua kuachana na kuendelea na maisha yetu kama marafiki," wawii hao wamesema kwenye taarifa yao ya pamoja. Amazon, ambayo imeanzishwa miaka 25 iliyopita wiki hii imeifunika Microsoft na kuwa kampuni yenye thamani kubwa zaidi duniani. Amazon ina thamani ya dola bilioni 797 baada ya soko la hisa la Marekani kufungwa siku ya Jumatatu baada ya kukua kwa asilimia 3.4 ikiipiku Microsoft ya Bill Gates yenye thamani ya dola bilioni 789. Bw Bezos, 54, ambaye ni mwanzilishi wa Amazon, ndiye mtu tajiri zaidi ulimwenguni kwa mujibu wa chati ya jarida mashuhuri la biashara la bloomberg , akiwa ...
BLESSED TO BLESS OTHERS