Skip to main content

Yusaku Maezawa: Bilionea wa Japan anayetafuta mpenzi wa kuandamana naye mwezini

Yusaku Maezawa

Yusaku Maezawa anajiandaa kuwa raia wa kwanza atakayesafiri mwezini kwa kutumia chombo cha Elon Musk


Bilionea wa Japan Yusaku Maezawa anamtafuta mwanamke atakayekuwa "mpenzi wa maisha" ili aandamane naye kutalii anga za mbali hadi mwezini.
Mwanamitindo huyo wa miaka 44, anajiandaa kuwa abiri wa kwanza kwenda mwezini kwa kutumia roketi maalumu inayofahamika kama ''Starship''.
Safari hiyo iliyopangiwa kufanyika mwaka 2023, itakuwa ya kwanza kwa binadamu kwenda mwezini tangu mwaka 1972.
Katika ombi la mtandaoni, Bw. Maezawa anasema kuwa anataka kufurahia safari hiyo na mwanamke wa kipekee.
Mfanyibiashara huyo ambaye hivi karibuni aliachana na mpenzi wake muigizaji Ayame Goriki mwenye umri wa miaka 27, ametoa wito kwa wanawake kuwasilisha maombi yao kuhusu"safari hiyo ya kipekee" katika tuvuti yake.
"Japo hisia ya upweke imeanza kunizonga, nafikiria kitu kimoja: kuendelea kumpenda mpenzi wangu," Bwana Maezawa aliandika katika tuvuti yake.
"Nataka kumpata 'mpenzi wa maisha'," Bwana Maezawa. "nikiwa na mpenzi wangu mtarajiwa wa maisha, nataka kuutangazia ulimwengu penzi letu nikiwa mwezini."


Presentational white space

Tovuti hiyo imeweka masharti pamoja na maelezo kuhusu jinsi ya kuwasilisha maombi katika mchakato huo utakaochukua miezi mitatu.
Masharti ya kushiriki lazima uwe bila mpenzi, uwe na miaka zaidi ya 20, uwe na mtazamo mzuri wa maisha na ufurahie kuzuru anga za mbali.
Muda wa mwisho wa kuwasilisha maombi ni Januari 17 ambapo uamuzi wa mwisho kuhusu mpenzi wa Bw. Maezawa utatolewa mwisho wa mwezi Machi.
Bilionea wa JapanI Yusaku Maezawa akizungumza karibu na roketi aina ya Falcon 9 wakati akitoa tangazo hilo, Septemba 17, 2018

Yusaku Maezawa anajiandaa kuwa raia wa kwanza atakayesafiri mwezini kwa kutumia chombo cha Elon Musk

Bilionea huyo ambaye amejizolea sifa kwa kuwa mpiga ngoma katika bendi ya punk, anajulikana kwa kujihusisha na visa ambavyo huzua gumzo na kuwaacha watu midomo wazi.

Mapema mwezi huu, Bw. Maezawa aliahidi kupeana yen milioni 100m sawa na ($925,000; £725,000) kwa watu 100 watakao share ujumbe wake wa twitter .
"Unachotakiwa kufanya ili kushiriki ni kunifuatilia kwa kutweet tena (Retweet)," alisema.
Mwanzilishi wa biashara tya kuuza nguo mtandaoni nchini Japan Zozo Inc, Bw. Maezawa alijizolea utajiri mkubwa katika ulimwengu wa uanamitindo.
Anaamniwa kuwa na utajiri wa karibu $3bn, sehemu kubwa ya pesa hizo anatumia katika Sanaa.










Comments

Popular posts from this blog

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...

Je unayafahamu maajabu ya Ziwa Ngosi Tanzania

Tanzania ni miongoni mwa nchi barani Afrika inayozungukwa na vivutio vingi vya utalii na vingine inawezekana hata havitambuliwi na wenyeji. Ziwa Ngosi yawezekana kuwa ni miongoni mwa vivutio hivyo. Ziwa hili ambalo ni la pili kwa ukubwa barani Afrika baada ya ziwa lingine la kreta lililopo Ethiopia linaakisi muonekano wa bara la Afrika katika upande wa kusini, magharibi, kaskazini na mashariki pamoja na visiwa vyake vya Unguja na Pemba.