Skip to main content

Nyota wa Afrika waliojumuishwa kwenye albamu ya Beyonce.

BEYONCE
Beyonce amefichua nyimbo zilizomo kwenye albamu yake mpya itakayoambatana na filamu mpya The Lion King remake na albamu hiyo imejumuisha wasanii nyota na wa juu wa muziki kutoka Afrika.
Wasanii wa Nigeria Tiwa Savage na Mr Eazi wanatumbuzia katika wimbo wa 'Keys to the Kingdom', wengine Tekno na Yemi Alade katika kibao 'Don't Jealous Me'.
Burna Boy ana kibao cha kipekee au solo, 'Ja Ara E', huku msanii wa Cameroon Salatiel akionekana akiimba na Beyonce na Pharrell Williams katika kibao 'Water'.

Wasanii wengine wa Afrika ni pamoja na Wizkid wa Nigeria, Shatta Wale wa Ghana, na Busiswa na Moonchild Sanelly kutoka Afrika kusini.
Alipotangaza mpango huo kwa mara aya kwanza wiki iliyopita, Beyonce alisema "Ilikuwa ni muhimu kuwa muziki usiimbwe na wasanii nyota na wenye vipaji bali iandaliwe na waandaaji wa Kiafrika. Ubora na moyo (mapenzi) vilikuwa vitu muhimu kwangu.
"Ni mchanganyiko wa kila kitu, si sauti moja tu. Kuna ushawishi kutoka kila kona, kutoka kwenye R&B, hip-hop na Afro Beat."


Tiwa savage
Msanii nyota kutoka Nigeria Tiwa Savage pia ameshirikishwa pamoja na Mr. Eazi katika kibao 'Keys to the Kingdom

Albamu hiyo ka jina 'The Lion King: The Gift', inatarajiwa kuzinduliwa Ijumaa hii.
Inajumuisha pia vibao vya ushirikiano na wasanii wa Marekani kama Kendrick Lamar, Pharrell Williams, Childish Gambino, na binti yake Beyonce, Blue Ivy miongoni mwa wengine.

Ni kibao tofauti kilichotumika kuisindikiza filamu hiyo ya The Lion King, Spirit, chenye mistari ya kiswahili, hatahivyo kimejumuishwa pia kwenye albamu hiyo.
Burna Boy




Wiki iliyopita, Beyonce aliachia kibao hicho kipya chenye maneno ya Kiswahili."Uishi kwa muda mrefu mfalme," sauti nyembamba inaimba kisha sauti nzito inaitika "uishi kwa", kionjo hiko kinajirudia mara mbili na kisha wimbo kuendelea kwa Kingereza.Filamu mpya ya Lion King imetengenezwa na kampuni kubwa ya Disney nchini Marekani.
Ujumbe wa Twitter wa @SteraClemond: A HUGE Congratulations to Busiswa & Moonchild for appearing on the New Beyoncé (The Lion King) Album. Representing South Africa 🙌🏼 🇿🇦 👑The Gift 🎶

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...