Skip to main content

ATM za maziwa yawakomboa wafugaji wa Kilimanjaro.











Maziwa ,kilimanjaro
Maziwa ,kilimanjaro






Nchini Tanzania wengi wao wanaposikia ATM kitu cha kwanza wanachoweza kufikiri huenda ikawa ni chombo cha kutolea fedha.
Jambo ambalo ni tofauti huko Kaskazini mwa Tanzania katika mkoa wa Kilimanjaro ipo ATM ya kwanza ya maziwa ambayo imeguka kivutio kwa wakazi wa mkoa huo.

Unaweza ukajiuliza ATM hiyo inafanyaje kazi?
Nancy Manase ni wenyekiti wa umoja wa wanawake wa maziwa
''Uone labda tulikuwa tunauza lita mia tatu kwa siku au mia nne sasa tumeongezea lita mia moja juu kwahiyo ni faida na msimu huu ni ule msimu unaokuwa na maziwa mengi sana huku kwetu maziwa yanakuwa mengi mpaka yanamwagwa kwahiyo mpaka sasa hivi hatujamwaga maziwa''.
ATM inatusaidia na watu wamepata elimu kunywa maziwa ni afya kwa sababu hata usipokula kitu kingine inakutosha''
Kila lita moja inagharimu wastani wa dola moja
Lakini katika mashine hii unaweza kununua maziwa ya kiwango chochote kulingana na hela ulionayo



Maziwa
Maziwa


''Kwa muda mfupi niliokuwa hapa katika ATM hii ya maziwa mkoani Kilimanjaro changamoto kubwa inayo ukabili mradi huu uliotokea kupendwa na walio wengi ni nishati ya umeme iwapo umeme utakatika basi ni vigumu kuipata huduma''


Wafugaji mmoja baada ya mwingine huleta maziwa yao hapa kwa ajili ya vipimo na kuandaliwa tayari kwenda kwenye ATM

Chakula na pesa
Mashine ya kununulia maziwa




Kwa upande wa wafugaji wanasema wameanza kuyaona matunda ya uwepo wa ATM hizi
Aleningwasa Swai ni mfugaji ambaye ananufaika na huduma hii.
"Maziwa yalikuwa hayana bei yalikuwa yananunuliwa kirojorojo tu, lakini tangu huu mradi ulipoanza wa kupeleka maziwa mjini tumepata faida sana , maziwa yanachukuliwa mwisho wa mwezi unakwenda kuchukua hela yako''.
Kwa wateja wa maziwa kwenye ATM nao walikuwa na maoni yao kuhusu mradi huu
"Maziwa ni mazuri nimeshakunywa maziwa sehemu nyingi, maziwa ya hapa nimeona kuna utofauti kidogo, cha kwanza maziwa yatoka kwenye ATM halafu istoshe maziwa ni mazuri kwa hiyo muda wote mtu ukihitaji maziwa ya kuchemsha na chai unapata muda wowote'', anaeleza mteja wa maziwa, Martin Karata
''Huduma hii ni nzuri ukija kwa muda wowote unapata maziwa, ikiwa asubuhi mchana jioni unapata maziwa,"Neema Munisi ni mteja pia.
Kwa sasa zipo ATM mbili tu kwa mkoa mzima
Na walio wengi wanatamani ziongezwe na kusambaa katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu
Kama kwenye vituo vya mabasi, Hospitalini na hata sokoni.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...