Skip to main content

As Roma kuzungumza na Waswahili kupitia Twitter

AS Roma Haki miliki ya picha AS Roma
Klabu ya mpira ya 'As Roma' nchini Italia imekuwa klabu kubwa ya kwanza kutoka barani Ulaya kuanzisha ukurasa wake katika mtandao wa Twitter.
Kurasa hiyo ya As Roma itakuwa ikiandika habari zake kwa lugha adhimu ya kiswahili.
Ukurasa huo wa lugha ya kiswahili ulizinduliwa rasmi jana, na inaaminika lengo kuu la 'As Roma' ni kuwafikia mamilion ya watu wanatumia lugha ya kiswahili. 
Akaunti hiyo ya Twitter imezinduliwa siku ya jumatano kwa video yenye maneno ya utani ya kiswahili.
Akaunti hiyo imepokelewa vizuri na wasomaji wa kiswahili wa Tanzania na Kenya.
Wengi wakiona kuwa ni ubunifu mzuri ambao unaonesha kuwajali mashabiki wanaoongea lugha ya Kiswahili.
Idadi kubwa ya watu wameanza kufuatilia kurasa hiyo na kujibu kwa kiswahili.
Rais wa klabu hiyo Jim Pallotta ametumia kurasa yake binafsi ya tweeter kuthibitisha kuwa kurasa hiyo imefunguliwa.
"Tuna furaha kuzindua kurasa ya kiswahili ya AS Roma", mkuu wa mipango Paul Rogers alieleza.
Uzinduzi huo umekuja mara baada ya kuzinduliwa kwa akaunti ya Pidgin
Juan Jesus

Mchezaji wa As Roma, Juan Jesus

H


Presentational grey line
Uzinduzi huu umekuja baada ya maombi ya mashabiki kutoka Tanzania, Kenya, Uganda, Afrika ya kati na mataifa mengine ya mashariki na kusini mwa Afrika.
Mapenzi ya soka la ulaya kutoka ukanda huu wa Afrika unastaajabisha kwa nini klabu za mpira za nje ya bara hilo kushindwa kuwasiliana kwa lugha ya kiswahili au Pidgin kabla ya mitandao ya kijamii.
"Kurasa hii ya Twitter itaturahisishia mawasiliano ya moja kwa moja na mashabiki wetu kwa namna ya kwao, ni mkakati ambao tunataka kuondoa vizuizi".
  • Akaunti mpya ya kiswahili ya AS Roma inawasiliana kwa lugha 14 tofauti katika mitandao ya kijamii.
Kuna kurasa nyingine rasmi za lugha ya kiitaliano, kiingereza, kiarabu,kifaransa, kireno, kichina, lugha ya Uturuki, Bosnian, , Dutch, Farsi na Pidgin.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...