Skip to main content

Watu nchini Uswizi washauriwa kuwavalisha mbwa wao viatu kuwakinga na joto la juu

A police dog in Zurich
Polisi katika mji wa Zurich nchini Uswisi wanawashauri watu kuwanunulia mbwa wao viatu ili kuwakinga kutokana na athari za viwango wa juu vya joto.
Kulingana na kituo cha habari cha kitaifa SRF, polisi mjini Zurich wamezindua kampeni ya kuwapa ushauri wafugaji wa mbwa, jinsi wanaweza kuwakinga kutokana na joto la juu, kutokana na sababu kuwa veranda na barabara zinaweza kuwa zenye joto.
Kiwango cha juu sana cha joto kimeshuhudiwa msimu wa sasa wa joto barani Ulaya, huku Uswizi ikishuhudia kiwango cha juu zaidi cha joto tangu mwaka 1864.
Kiwango cha joto mwezi Julai kilifikia nyuzi 30.
Kulingana na msemaji wa polisi Michael Walker, nyuzi 30 ni sawa na kati ya nyuzi 50-55 ardhini au kwenye lamu kutokana na hali kwamba ardhi huhifadhi joto.

Comments