Skip to main content

KAZI NNE ZINAZOLIPA MISHAHARA MIKUBWA TANGU AWALI.

Je wajua baadhi ya wahitimu wapya wanaanza taaluma zao kwa mishahara ambayo wafanyikazi wengi hawatawahi kufikia katika taaluma zao? Davis Nguyen, anawasaidia waliohitimu vyuoni kuanza taaluma zao kupitia ushauri wa usimamizi. Ni tasnia ambayo kihistoria imekuwa ikilipa vizuri: hata kabla ya janga la corona, kuna baadhi ya kampuni kubwa ambazo ziliwalipa wahitimu mishahara mikubwa zaidi. Lakini, katika soko la sasa, wateja wa Nguyen wanafanya vizuri sana. “Watarudi na kusema ‘Nina ofa mbili kuu’,” aeleza mwanzilishi huyo wa My Consulting Offer, iliyoko Georgia, Marekani. "Moja ni dola elfu 120, nyingine ni dola elfu140. Mazingira ya leo inamaanisha wahitimu wanaweza kupata pesa nyingi zaidi kuliko miaka michache iliyopita.



Tafadhali fuatilia makala haya yanayo chambua kwa kina taaluma hizi mpaka mwisho ikiwa wewe una malengo ya kukuza malipo yako.
    1.USHAURI WA USIMAMIZI

Hii ni mojawapo wa taaluma ambazo wahitimu wanazidi kwenda moja kwa moja kutoka darasani hadi katika kazi zinazolipa vizuri - kupata mshahara ambao baadhi ya watu hawatawahi kuziona maishani mwao.

Washauri wa usimamizi husaidia makampuni kutatua matatizo, kuimarisha utendaji wa biashara, kuzalisha thamani, na kuongeza ukuaji.

Kazi inayofanywa na washauri wa usimamizi inaweza kutofautiana, ambayo ni pamoja na biashara ya kielektroniki, uuzaji, usimamizi wa ugavi na mkakati wa biashara.

Kazi za kila siku za kazi ni pamoja na kufanya uchambuzi wa takwimu thabiti; mahojiano na wafanyikazi wa mteja; kuwasilisha na kuunda mapendekezo ya biashara, pamoja na kusimamia timu, kusimamia utekelezaji wa mapendekezo haya.

    


    2.UCHAMBUZI WA DATA. 

Mchambuzi wa data mara nyingi kuzingatia mbinu za utafiti wa takwimu usindikaji wa data ya takwimu na uchambuzi wa matokeo ili kupata hitimisho la busara.

Katika mashirika makubwa zaidi ya benki, malipo ya wachambuzi wa mwaka wa kwanza yameongezeka kwa karibu 30% - mshahara wa msingi wa dola elfu 110 sawa na (£83,979),mara nyingine.




3. UWAKILI.

Wakili ni mtu ambaye alisomea sheria na kufundishwa kama mtaalamu wa sheria. Yeye ni mtaalam wa sheria na nambari za kisheria, kwa hivyo ana sifa ya kuwakilisha, kusaidia, kushauri, kutetea na kusimamia taratibu mbele ya mashirika ya umma na ya kibinafsi, kwa kuzingatia haki na masilahi ya raia ambao wanaomba huduma zake.

Katika makampuni makubwa ya sheria ya London, baadhi ya mawakili wapya waliohitimu huanza kazi zao kwa malipo ya mshahara wa pauni elfu 107,500 sawa na (dola141,115).

Nguyen anasema "vijana walioa na umri wa miaka 20 wanalipwa mshahara wa dola elfu 100,000 wameongezeka" na hiii imezidi kuwa jambo la kawaida tangu janga la corona lilipokumba ulimwengu.



3. UHANDISI WA KOMPYUTA.

Siku hizi, vifaa vya kompyuta vimewekwa katika bidhaa nyingi za elektroniki, na ulimwengu umeunganishwa kupitia mifumo ya kompyuta.

Kwamujibu wa mtandao wa wa Try Engineering, kazi ya mhandisi wa kompyuta inategemea vifaa  -inazingatia mifumo ya uendeshaji na programu.

Wahandisi wa kompyuta lazima waelewe muundo wa kimantiki, muundo wa mfumo wa microprocessor, usanifu wa kompyuta, upatanishi wa kompyuta, na waendelee kuzingatia mahitaji na muundo wa mfumo.

Kwa hiyo wahandisi wa kompyuta wanafanya kazi katika kila aina ya viwanda na kuendeleza na kuunganisha bidhaa na mifumo kwa njia mpya kila siku.

Katika Kampuni kubwa za teknolojia, wahandisi wa programu za kiwango cha awali mara nyingi huanza kwa mishahara mikubwa.


                                                                                                                      

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...