Skip to main content

Fahamu ukweli wa dhana tano kuu kuhusu nyoka na maadhimisho ya nyoka duniani

nyoka msituni

Huku Tarehe 16 mwezi Juni ikiwa ni siku ya maadhimisho ya siku ya nyoka duniani mnyama huyo hutazamwa kwa hatari kubwa, waerevu na mara nyingine hata kuhusishwa na imani potofu na uchawi katika baadhi ya jamii za Kiafrika.

Kwa kawaida nyoka anakuwa juu ya orodha ya mambo ambayo mtu anaogopa maishani mwake.

Maelfu ya watu duniani hufariki kutokana na sumu kali ya nyoka baada ya kuumwa kila mwaka kwa mujibu wa shirika la afya duniani.

Ukosefu wa matibabu na hata matibabu mabaya hufanya vifo hivyo kutokingika.

Kuumwa na nyoka huenda kusionekane kuwa janga baya la kiafya.

Lakini katika maeneo mengine duniani ni hatari kila siku na huenda kukasababisha maafa ama hata kubadilisha maisha ya mtu.

Pengine ndio sababu ya kuwepo dhana tofuati, baadhi potofu, kuhusu wanyama hawa.

Hebu tuwafahamu zaidi.

Nyoka mdogo aina ya pit viper
Maelezo ya picha,

Nyoka mdogo aina ya pit viper

Je ni kweli?

Nyoka hawatambai kwenye mawe na kamba

Wanaweza kutambaa juu na hata chini ya mawe, kwenye miti na majengo. Nyoka hupenda kujificha ardhini.

Ni rahisi kwao kujificha chini ya vichaka, na vigumu kutambaa chini ya mawe madogo kwenye bustani.

Ni vyema kuzikata nyasi ziwe ndogo na uondoshe masalio yoyote ya nyasi zilizokatwa au majani makavu yalioangukana kujikusanya.

Kadhalika ni vymea uondoshe sehemu za mti zilizoanguka juu ya paa au zinazoning'inia kutoka nyumba yako.

Ukiona mtoto wa nyoka na familia nzima i papo

Iwapo nyoka huzaa watoto au kutaga mayai, kawaida anapojifungua huwaondokea watoto na kuwaacha kivyao.

Iwapo utamuona nyoka mkubwa karibu na mdogo basi huenda ni sadfa tu.

Wao hutawanyika punde wanapojifungua.

Eyelash viper
Maelezo ya picha,

Eyelash viper

Nyoka huteleza

Kawaida, watu ambao hawajawahi kumgusa nyoka hudhani kwamba wanyama hao huteleza ukiwagusa. Ngozi ya nyoka huonekana kuwa kavu, lakini kwa kuigusa ni nyororo.

Nyoka ni wakali

Nyoka wanaogopa binaadamu zaidi ya binaadamu wanavyowaogopa. Kwa kawaida huwa wana haya au aibu sana na iwapo wangekuwa na nafasi anaweza kutoroka asionekane.

Ni iwapo tu amekwama au ametishiwa, kama ilivyo kwa kiumbe chochote, nyoka hushambulia kujilinda.

Lakini mara nyingi baadhi huona afadhali kutoroka kuliko kushambulia.

Nyoka wote hutaga mayai

Licha ya kwamba reptilia wengi hutaga mayai, sio nyoka wote wanaotaga. Baadhi ya nyoka kama wa aina ijulikanayo kama Oriental Vine, huzaa nyoka wadogo.

Mfahamu zaidi Nyoka

  • Je unafahamu kwamba kuna zaidi ya aina 3000 za nyoka duniani?
  • Kati yao, 375 wana sumu.
  • Nchini Australia, kuna aina 140 za nyoka na 100 huwa na sumu.
  • Nyoka mwenye sumu kali duniani ni wa Australia - Inland Taipan.
  • Nyoka huwa na urefu wa kati ya sentimita 10 mpaka mita 7 aina ya chatu.
  • Nyoka huishi katika mazingira tofauti ikiwemo vichaka, jangwani na hata ndani ya maji.
         Hutumia ulimi wao kumnusa adui kabla ya kumshambulia.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...