Skip to main content

Posts

Showing posts from May, 2019

Mambo 8 muhimu ya kukusaidia kufaulu katika usaili wa kazi

kijana akiwa kwenye usaili wa kazi Kupata kazi ya ndoto zako si jambo jepesi, na inawezekana ikawa ni vigumu zaidi kama hujui waajiri wanataka nini kutoka kwako. Ulimwengu wa wa ajira - kwa kampuni kubwa na ndogo - unabadilika kwa kasi sana. Lakini kuna eneo moja ambalo ni la muhimu kuzingatiwa kwa kila msaka ajira: usaili wa ana kwa ana. "Usaili huo ni sehemu kubwa zaidi ya mchakato wa ajira," amesema Jane Tippin, ambaye ni gwiji wa masuala ya rasilimali watu ambaye hutumiwa na kampuni kubwa ya benki nchini Uingereza ya Lloyds Bi Tippin anaamini kuwa uwezo wako wa kujibu maswali mbele ya mtu ama jopo la watu linaweza kujenga ama kubomoa mustakabali wako wa kupata ajira. Hivyo, unahitajika kujiandaa kikamilifu kabla ya kuingia kwenye chumba cha usaili wa ana kwa ana. Zifuatazo ni dondoo muhimu zitakazokusaidia kufaualu usaili huo: 1. Fanya utafiti. ...

Ujumbe wa mahaba wa Reginald Abraham Mengi kwa mkewe Jacqueline Ntuyabaliwe-Mengi kabla ya kifo chake

Haki miliki ya picha K Marehemu Reginald Abraham Mengi, ambaye ni bilionea na mfanyibiashara mkubwa nchini Tanzanian alichapisha ujumbe wa mahaba kwa mkewe Jacqueline Ntuyabaliwe-Mengi katika mtandao wa Twitter akimuelezea jinsi anavyompenda. Katika ujumbe huo wa kuadhimisha miaka minne tangu wawili hao wafunge ndoa yao mwaka 2015, bilionea huyo alisema: Ni furaha kuadhimisha ndoa yetu mpenzi wangu. Imekuwa safari iliojawa na mapenzi na furaha. nakupenda sana, aliandika bilionea huyo. Ruka ujumbe wa Twitter wa @regmengi Happy Anniversary My Sweet love. It has been a very exciting journey full of love and happiness. I love you crazy.  pic.twitter.com/ly89d4Jlh7 — Reginald Mengi (@regmengi)  28 Machi 2019 Mwisho wa ujumbe wa Twitter wa @regmengi Ujumbe huo ulimfurahisha mkewe aliyewahi kuwa malkia wa urembo wa Tanzania na ambaye aliujibu kwa kumhakikishia mapenzi tele: Wewe ndio mwanamume wa pekee ambaye ningependelea kuishi maisha yangu nawe , mtu ambaye ...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...