Skip to main content

Posts

Showing posts from March, 2019

Rais asiyeonekana mbele za watu Abdelaziz Bouteflika atawezaje kuiongoza tena Algeria?

Haki miliki ya picha AFP Image caption Hotuba ya wazi inayofahamika kutoka kwa Rais Bouteflika ilikua mwaka 2014 Kwa raia wengi wa Algeria ni vigumu kuelewa ni kwa vipi rais wao mwenye miaka 82 ,aliyeugua kiharusi miaka sita iliyopita na kupata shida kwenye kutembea au kuzungumza anaweza kuongoza nchi. Hakuna aliyeamini ilipotangazwa kuwa Abdelaziz Bouteflika anawania awamu ya tano mwezi Aprili-hata mwenyewe hakujitokeza binafsi siku ya Jumapili kujisajili kuwania nafasi hiyo . Waalimu, wanafunzi, wanasheria hata waandishi wa habari waliingia mitaani kuandamana wakiwa na hasira , walionekana kutokubaliana na hatua ya kuongozwa na mtu ambaye haonekani. Wengi wanahofu kuwa kutopatikana kwa mrithi wa Rais Bouteflika, ambaye aliingia madarakani mwaka 1999, kunaweza kusababisha hali ya usalama kuyumba nchini humo. Kiongozi wa kwenye TV Kwa mara ya mwisho alionekana akihutubia Umma mwaka 2014 -hotuba ya shukrani kwa raia wa Algeria kwa kuuamini utawala wake baaa ya kushinda uchagu...

Shambulio katika misikiti ya Christchurch: Watu 49 wameuawa katika shambulio la kigaidi New Zealand

Haki miliki ya pic EUTERS Image caption Emergency services personnel transport a person on a stretcher Waziri mkuu wa New Zealand Jacinda Ardern anasema watu 49 wameuawa na wengine zaidi ya 20 wamejeruhiwa vibaya baada ya kuzuka mashambulio katika misikiti miwili katika mji wa Christchurch, huko New Zealand. Waziri mkuu huyo amelitaja shambulio hilo kuwa mojawapo lililotanda 'kiza kikubwa' siku ya leo nchini humo. Wanaume watatu na mwanamke mmoja wamekamatwa, kamishna wa polisi Mike Bush anasema, lakini ameonya kwamba huenda washukiwa zaidi wapo. Inaarifiwa kwamba washambuliaji hao hawakuwa kwenye orodha ya magaidi wanaosakwa lakini ni wazi kwamba wana itikadi kali. Waziri mkuu wa Australia Scott Morrison amesema mojawapo ya waliokamatwa ni raia wa Australia. Amemtaja mshukiwa wa shambulio hilo kuwa "gaidi mwenye itikadi kali za mrengo wa kulia". Walioshuhudia mkasa huo wameambia vyombo vya habari kwamba walilazimika kutoroka kuokoa maisha yao na walion...

Karl Lagerfeld: Mbunifu wa mitindo amrithisha paka wake Choupette sehemu ya utajiri wake wa mamilioni ya dol

Taarifa zimeibuka kwamba mbunifu mavazi aliyeaga dunia Karl Lagerfeld amemuachia paka wake sehemu ya utajiri wake wenye thamani ya $ milioni 200. Mbunifu huyo, raia wa Ujerumani, ambaye alikuwa mbunifu mkurugenzi wa kampuni za Chanel na Fendi, alifariki Paris Jumanne. Alimlea paka wake wa dhati na alivutia ufahari aliokuwa nao kwa paka wake Choupette tangu alipokabidhiwa mnamo 2012. Lagerfeld ameliambia jarida la Ufaransa Numero mwaka jana  kwamba amemueka paka huyo kwenye wasia wake kama mmoja wa warithi wa makaazi yake ya kifahari. Katika mahojiano hayo, alisema Choupette yumo ndani ya urathi, 'miongoni mwa wengine'. Lakini ameongeza : "Usijali kuna mali ya kumtosha kila mtu." Haki miliki ya pich GES Image caption Lagerfeld akiwa karibu na mchoro wa Choupette Tayari Choupette ana utajiri wa kiasi, akiwa amejipatia $ milioni 3 kutokana na matangazo ya biashara kwa kampuni ya magari Ujerumani na kampuni ya vipodozi ya Japan akiwa na mmiliki wake Lagerfeld. ...

Boeing 737 Max: Rwanda yapiga marufuku hizo kuruka katika anga yake

Haki miliki ya picha STEPHEN BRASHEAR Shirika la usafiri wa ndege Rwanda limetoa agizo kwa marubani na kampuni za ndege kutoendesha ndege za Boeing 737 Max 8 ana 9 katika anga ya Rwanda. Rwanda sasa imejiunga na mataifa mengine duniani ambayo yamepiga marufuku usafiri wa ndege hizo za aina ya Boeing 787 Max 8 na Max 9. Hii inafuata ajali ya ndege ya Ethiopia Airlines Jumapili ilioanguaka muda mfupi baada ya kupaa kutoka mji mkuu Addis Ababa na kusababisha vifo vya watu 157 Taarifa zinaeleza kwamba Rwanda ilikuwa na mipango ya kukodisha ndege mbili za aina hiyo Boeing 737- 800. Hatahivyo, huenda mipango hiyo ikasitishwa kwa muda sasa wakati kukisubiriwa uchunguzi wa chanzo cha ajali ya ndege ya Ethiopia iliyoanguka Jumapili nje kidogo ya mji mkuu Addis Ababa. Ndege kama hiyo ya kampuni ya Lion Air, ilianguka kutoka pwani ya Indonesia Oktoba mwaka jana na kusababisha vifo vya watu 189. Katika taarifa rasmi iliyowekwa kwenye mtandao wa twitter ya mkurugenzi mkuu katika shirik...