Skip to main content

Posts

Showing posts from August, 2018

Nidhamu ya matumizi ya simu: Mambo matano ya kukuepusha kuwakera wengine

Ni kitu cha kwanza wengi wetu tunakitazama asubuhi na kitu cha mwisho kukiangalia usiku.Simu zetu haziko mbali nasi na tunaziangalia kila baada ya dakika 12, kwa mujibu wa mamlaka ya kudhibiti mawasiliano nchini Uingereza, Ofcom. Ni mahusiano ambayo yanaonekana kuwa yatadumu zaidi, hivyo tunakudokeza sheria tano za matumizi ya simu ambayo yanapaswa kutazamwa kwa umakini. 1. Kuzungumza na simu wakati wa kula chakula Watu wengi hufanya hivyo, na zaidi ya 26% ya vijana wanakubali suala hili ''Simu zinapaswa kuwa zimezimwa saa zote wakati wa chakula, mikutano na sherehe,''anasisitiza Diana Mather, mshauri wa masuala ya tabia. ''Mtu uliyenaye ni mtu aliye muhimu zaidi.Hakuna miongoni mwetu asiye na umuhimu. Hata kutazama televisheni inakuwa imezimwa kwa baadhi ya watu wakati mkiwa kwenye meza ya chakula Zaidi ya watu wanne kati ya watano walio na umri wa miaka 55 na zaidi wanafikiri haikubaliki kutazama ujumbe wa simu ukilinganisha na 46% ya umri wa...

Watu nchini Uswizi washauriwa kuwavalisha mbwa wao viatu kuwakinga na joto la juu

Polisi katika mji wa Zurich nchini Uswisi wanawashauri watu kuwanunulia mbwa wao viatu ili kuwakinga kutokana na athari za viwango wa juu vya joto. Kulingana na kituo cha habari cha kitaifa SRF, polisi mjini Zurich wamezindua kampeni ya kuwapa ushauri wafugaji wa mbwa, jinsi wanaweza kuwakinga kutokana na joto la juu, kutokana na sababu kuwa veranda na barabara zinaweza kuwa zenye joto. Kiwango cha juu sana cha joto kimeshuhudiwa msimu wa sasa wa joto barani Ulaya, huku Uswizi ikishuhudia kiwango cha juu zaidi cha joto tangu mwaka 1864. Kiwango cha joto mwezi Julai kilifikia nyuzi 30. Kulingana na msemaji wa polisi Michael Walker, nyuzi 30 ni sawa na kati ya nyuzi 50-55 ardhini au kwenye lamu kutokana na hali kwamba ardhi huhifadhi joto.

Je kati ya Neymar na Mbappe nani anayepigiwa upatu kushinda taji la Ballon d'Or

Neymar alipojiunga na Paris St-Germain kwa dau lililovunja rekodi ya £200m msimu uliopita alionekana kuwa mchezaji ambaye atavunja utamaduni wa kushinda taji la Ballon d'Or ambalo Messi na Ronaldo wamekuwa wakishinda.Lakini wiki nne baadaye kijana nyota Mbappe alijiunga na PSG kwa mkopo kutoka Monaco kabla ya uhamisho huo kuwa wa kudumu baada ya Monaco kulipwa £165.7m."Huku Kylian Mbappe na Neymar, wakiwa washambuliaji bora zaidi duniani katika klabu ya PSG ,mwandishi wa gazeti la Le Parisien Yve Leroy aliambia BBC Sport ,'' wote wanawania taji la mchezaji bora duniani huku ikijdaiwa kwamba huenda Cristiano Ronaldo na Messi wasishinde"