Marekani imesema kuwa imemuorodhesha mwana wa mwisho wa Osama Bin Laden, Hamza, katika orodha ya magaidi wanaosakwa na taifa hilo. Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema kuwa Hamza Bin Laden ameanza kushiriki katika maswala ya kundi la al Qaeda, kundi la jihad lililofadhiliwa na babake. Amesema kuwa atalipiza kisasi mauaji ya babake yaliotekelezwa na kikosi maalum cha Marekani kwa kutekeleza mashambulizi dhidi ya Wamarekani. Osama aliacha dola milioni 29 kufadhili Jihad Mzozo kuhusu shamba la Osama Pakistan Sasa atapigwa marufuku kwa kufanya biashara na raia wa Marekani huku mali yake ikipigwa tanji. Mamake Hamza ni Khairiah Sabar, mmoja wa wake za Osama aliyekamatwa wakati wa shambulio la wanajeshi wa Marekani kwenye maficho ya Osama mjini Abbotabad nchini Pakistan mwaka 2011. Mkuu wa kitengo cha usalama cha kundi la al-Qaeda Ibrahim al-Banna pia ameongezwa katika orodha hiyo . Marekani imetoa kitita cha dola milioni 5 kwa mtu yeyote atakayemkamata al-Banna. ...
BLESSED TO BLESS OTHERS