Skip to main content

Posts

Showing posts from September, 2016

Nyoka atafuta' joto' kwenye kiatu Australia

Mwanamke wa Australia amewaita maafisa wa wanyama pori kumtoa nyoka wa urefu wa mita 1 mwenye sumu kali kutoka kwenye kiatu chake. Mnasa nyoka Rolly Burrell alimdhibiti nyoka huyo wa rangi ya chokoleti aliyekuwa anatafuta ''joto'' nyumbani mwa mwanamke huyo Adelaide, kusini mwa Australia. Alikuwa ametoka nje ya nyumba yake iliopo mashambani kukusanya viatu vyake na hapo akaona mkia ukipotea ndani ya kiatu chake kimoja. Nyoka huyo ni mmoja wa wanaoonekana kuwa wenye sumu kali duniani na hupatikana katika pwani na maeneo ya ndani ya ardhi kavu Australia "Alitoka nje kuchukua viatu vyake na akaona kitu kikitoweka kwa kasi, ALISEMA Rolly Burrel "Aligundua kuwa ni nyoka." Nyoka huyo ambaye ni aina inayopenda kujificha, alichiliwa msituni kando na mbali na maenoe ya makaazi ya watu . Bwana Burrell amesema kampuni yake iliitwa kwa mara nyengine kutoa nyoka kwenye kiatu takribana mwaka mmoja uliopita. Viatu hivyo aina ya buti, vimetengenezwa kwa...

Je Giggs amezea mate kuwa meneja wa Swansea?

Ryan Giggs huenda anapendelea kuwa meneja wa klabu ya Swansea ikiwa kiongozi wa sasa Francesco Guidolin ataachia ngazi kama tetesi zinavyobashiri. Giggs, mwenye umri wa 42, aliihama Manchester United kama meneja msaidizi tangu July - na kumaliza uhusiano wake wa miaka 29 na klabu hiyo. Swansea tayari imepata pointi 4 kutoka kwa mechi 5 walizocheza msimu huu lakini inasemekana klabu hiyo ya Wales ina mpango wa kubadili uongozi. Sio kwamba Giggs ndio chaguo pekee la Swansea iwapo mabadiliko hayo yatafanyika. Isitoshe, tangu alivyoondoka Old Trafford , Giggs amekuwa akiendeleza zaidi biashara zake za siku nyingi kwenye maswala ya matangazo ya biashara ya TV work na pia katika Salford City, klabu ambayo anaimiliki pamoja na watimu wenzake wa zamani Paul Scholes, Nicky Butt, Gary na Phil. Awali Giggs alionesha hamu ya kumrithi Louis van Gaal kama meneja wa Manchester United lakini naibu mwenyekiti Ed Woodward badala yake akamchagua Jose Mourinho baada ...