Skip to main content

Gwaride maalum China litakaloonyesha silaha zake mpya

A row of Chinese soldiers shouting during marching drills Haki miliki ya picha
China itakuwa na gwaride kubwa la kijeshi hapo kesho kwa ajili ya kusheherekea miaka 70 ya chama kinachotawala nchini humo cha 'Communist' , na nchi hiyo imehaidi kuonyesha silaha mpya zinazotengenezwa nchini humo katika mji wa Beijing.
Je, ni silaha gani watakazozionyesha na kwanini China sasa inatambuliwa kama taifa la pili lenye bajeti kubwa ya kijeshi duniani?
Oktoba mosi kuna mipango gani?
Gwaride la kijeshi ni miongoni mwa mambo makubwa yatakayofanyika katika sherehe hiyo kubwa itakayofanyika katika eneo la Tiananmen litahudhuriwa na maafisa wakubwa, wananchi kadhaa walioallikwa na askari 188 kutoka nchi 97.
Two people take a selfie in Tiananmen Square Haki miliki ya pich
Image caption Pamoja na shauku kubwa iliyopo miongoni mwa watu lakini ni watu wachache u ndio watapata nafasi ya kuhudhuria
Msemaji wa waziri wa ulinzi alisema hivi karibuni kuwa China haina mpango au haiitaji kuonyesha nguvu iliyonayo lakini wamelenga kuonyesha upendo, amani na namna China inawajibika.
Gwaride hili limelenga kuwavutia wengi na litatumika kuonyesha vitu.
Wizara ya uinzi imeripoti kuwa wanajeshi 15,000 watashiriki pamoja na 59 ambao watatoka vikosi mbalimbali , huku silaha 580 zitaonyeshwa katika mitaa mbalimbali na ndege za kijeshi 160 zitarushwa angani.
Rais Xi Jinping atakagua gwaride hilo katika makutano ya Chang'an mjini Beijing na baada ya hapo ndege za jeshi zitaruka katika eneo la Tiananmen.
Kwa mara ya kwanza, askari 8,000 kutoka China ambao walikuwa mashujaa wa ulinzi wa amani wa Umoja wa mataifa wataweza kushiriki.
Ni Silaha gani tutaziona?
Jeshi la 'People's Liberation Army (PLA)' lina shauku ya kuonyesha silaha mpya katika hadhara ambazo zimeshaanza kutumika.
Aircraft fly in formation over Beijing releasing coloured smoke - 2015
Haki miliki ya pich


Image caption Maadhimisho yaliyofanyika mwaka 2015
Miongoni mwa silaha ambazo zinatarajiwa kuoneshwa:
  • Silaha mpya ya DF-41 ambayo wachambuzi wanasema kuwa imelenga kutumika sehemu yoyote ulimwenguni itaweza kuonyeshwa.
  • Silaha nyingine ni MIRV ambayo ina muongozo maalumu wa ufanyaji kazi, ina uwezo wa kupiga maeneo 10 tofauti katika eneo kubwa .
  • Mashine nyingine ni DF-17, inatajwa kuwa gari kubwa lenye uwezo wa kubeba mzigo mkubwa na ina kasi kubwa.
  • Silaha nyingine mpya za magari, ndege na meli za kijeshi zitaweza kuonyeshwa.
  • Two unmanned aircraft Ndege mbili za kijeshi ambazo hazikutajwa majina zikiwa na muundo wa ndege isiyokuwa na rubani pia zitaonyeshwa ingawa zinalengwa kuitwa DR-8 .
A Chinese J-20 stealth fighter performs at the Airshow China 2018 in Zhuhai Haki miliki ya picha
  • Y-20 ni ndege ya kijeshi ambayo ina uwezo wa kutoa angalizo kwa watumiaji
Servicemen post in front of a H6-N strategic bomber Haki miliki ya picha
H6-N ni aina mpya ya bomu nchini China ambayo ina uwezo wa kufanya milipuko kadhaa angani.
PLA imesisitiza kuwa itaonyesha uvumbuzi waote mpya uliofanyika nchini humo katika sekta ya ulinzi na namna maboresho walioyafanya.
Ni gharama gani inatumika katika jeshi la China?
Gharama inayotumika katika jeshi la China inazidi kuongezeka tangu rais wa nchi hiyo kutangaza kufanya maboresh mwaka 2015.
Zaidi ya muongo, bajeti ya wizara ya ulinzi imeongezeka kwa asilimia 10 kila mwaka na sasa bajeti hiyo kufikia dola $168.2bn hivyo kufanya taifa hilo kuwa la pili duniani.
Graph showing US military spending at $643bn and China at $168bn
China ina uwekezaji mkubwa zaidi wa ulinzi barani Asia mwaka 2018 kwa kutumia $56.1bn kwa silaha na utafiti wa usalama na maendeleo, ambapo ni sawa na zaidi ya asilimia 33 ya bajeti ya ulinzi nchini China.
Matokea ya hivi karibuni ya matumizi na sababu ya matumizi hayo imeandikwa katika wizara hiyo. 
Kwa msisitizo wa idara hiyo ya usalama, matumizi ya China yamefananishwa na matumizi ya Marekani ambayo bado iko juu kwa jumla ya bilioni $643.3b kwa mwaka 2018.
Pamoja na kwamba China ni nchi ya pili kwa uchumi mkubwa duniani lakini wizara ya ulinzi ilitumia robo ya kile kilichotumika Marekani mwaka 2017, na imefanya kazi kwa $100 kwa kila mtu ambayo sawa na 5% ya Marekani.
China inafikiria kutumia vipi jeshi lake?
China inasema kuwa mpango wake wa kutengeneza jeshi lenye nguvu ni kutaka kuendelea kuwa katika vigezo vya kimataifa na kuongoza kuwa na jeshi linaloongoza duniani .
Chinese peacekeeping troops walk along a road in South Sudan Haki miliki ya picha
Image caption China imesisitiza jukumu la kulinda amani duniani katika miaka ya hivi karibuni
China imeweza kutengeneza kisiwa huko kusini mwa China mwishoni mwa mwezi june kwa ajili ya jeshi.
Satellite image of Chinese military build-up on Fiery Cross Reed in the Spratly Islands Haki miliki ya pi
Eneo hilo limetengeza mfumo wa (A2AD) linaaminiwa kuwa lina uwezo wa kuzuia Marekani kuingia kusini mwa China kutokea ufukweni mwa bahari.

Je, China inakaribia kuipita Marekani?

Moja ya tofauti kubwa ambayo itaonekana hapo kesho katika gwaride la maadhimisho haya na ya mwaka 2015, ni sherehe za angani.
Chinese troops practice with anti-aircraft guns during drills Haki miliki ya picha
Ikiwa China inaadhimisha miaka 70 ya ushindi kati yao na Japan katika vita ya pili ya dunia.
Gwaride linaangazia kusheherekea mafanikio ambayo China yameyapata katika upande wa uvumbuzi na utengenezaji wa bidhaa mbalimbali.
Taifa hilo linataka kuwa na jeshi kubwa la kisasa zaidi duniani kwa mwaka 2035 na jeshi bora zaidi ifikapo mwaka 2049.
Pamoja na matarajio yote mazuri, yanahitaji uwekezaji mkubwa zaidi.
China inahitajika kuboresha malipo ya wanajeshi, kuwa na mafunzo mambo ambayo yatagharimu pakubwa.

Comments

Popular posts from this blog

Kiongozi wa Republican ahofia uongozi wa Trump

Kiongozi mmoja wa chama cha Republican nchini Marekani amesema kuwa anahofia maisha ya wajukuu wake saba ,chini ya uongozi wa rais mteule wa Marekani Donald Trump. Christine Todd Whitman ,ambaye ndio mkuu wa shirika la kulinda mazingira nchini Marekani amemshtumu Donad Trump kwa kupuuza ripoti za sayansi. Na amenonya kwamba tishio lake la kuondoa sera za kulinda hali ya anga linaweka siku za usoni hatarini. Wafuasi wa Trump wanasema kuwa sheria za hali ya anga na kawi zinaharabu biashara. Lakini Bi Todd Whitman amesema kuwa Marekani inapaswa kutafuta njia za kukuza biashara bila kuharibu mazingira. Maelezo kuhusu sera za mazingira za bw Trump hayajulikani ,lakini wanaomzunguka wanasema kuwa analenga kuimarisha mkaa, kufungua mabomba mapya ya mafuta, na kuruhusu uchimbaji madini msituni mbalii na kuchimba mafuta katika eneo la Arctic. Kisiasa ,wamependekeza kujiondoa katika makubaliano ya hali ya anga, kufutilia mbali sera ya rais Obama ya kupata kawi safi mbali na k...

Wasifu wa Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi au K-Lynn

Haki miliki ya picha JACQUELINE NTUYABALIWE  Jacqueline Ntuyabaliwe (Jacqueline Ntuyabaliwe Mengi) ambaye pia anajulikana kama K-Lyn alizaliwa tarehe 6 mwezi Disemba 1978 mjini Dar es Salaam, Tanzania. Ni Mwanamuziki , mfanyabiashara na aliwahi kushinda taji la malkia wa Urembo nchini Tanzania (2000). Ni Mwanzilishi wa kampuni ya samani ilioshinda tuzo Amorette Ltd . Babake alitoka kutoka eneo la Kigoma akiwa daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake huku mamake akiwa nesi. Alisomea elimu yake ya msingi katika shule ya bweni ya Nyakahoja Primary mjini Mwanza kabla ya kuelekea mjini Dar es Salaam ambapo aliendelea na elimu yake ya msingi katika shule ya Forodhani. Jackline ni msichana wa mwisho katika familia ya watoto watatu wa kike Katika utoto wake alikuwa msichana mwenye haya jingi lakini alipendelea sana kusoma vitabu Muziki Alianza usanii 1997 akishirikiana na bendi ya Tanzania kwa jina the Tanzanites. Aliimba kama mmojawapo wa viongozi kwa miaka mitatu. ...

Mwanza: Kibao kipya cha nyota Rayvanny na Diamond Platnumz chafungiwa na Basata

Kibao kipya kiitwacho, Mwanza, kilichotolewa na wasanii mashuhuri Tanzania Rayvanny na Diamond Platnumz kimepigwa marufuku na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata). Katika taarifa kwa umma iliyotolewa leo Novemba 12 Katibu Mtendaji wa Basata Godfrey Mngereza, sababu kuu ya kufungiwa wimbo huo ni ukiukwaji mkubwa wa maadili ya Kitanzania kwa "kutumia maneno yanayohamasisha ngono." Basata pia imeonya vyombo vya habari, na watu binafsi kutoutumia, kuucheza ama kuusambaza wimbo huo kwa namna yoyote ile. "Baraza linatoa onyo kali kwa msanii Rayvanny, Diamond Platnumz pamoja na uongozi wa Wasafi Limited kufuata sheria, kanuni na taratibu wakati wa kuandaa kazi za sanaa. Aidha Baraza limesikitishwa na kitendo hiki ambacho kimefanywa kwa makusudi," imeeleza taarifa hiyo iliyosainiwa na Mngereza. Wimbo huo wa Mwanza ulitolewa rasmi jana na tayari ulishavutia maelfu ya watazamaji kwenye mitandao ya kijamii. Wasanii hao wametakiwa kufuta kibao hiko katika kurasa...