Skip to main content

Posts

Showing posts from July, 2016

Mtoto apandikizwa pua mpya India

Madaktari nchini India wamepandikiza pua mpya katika uso wa mvulana wa miaka 12 iliokuwa imemea katika paa lake la uso. Pua ya Arun Patel iliharibika alipougua ugonjwa wa homa ya kichomi Maambukizi hayo yaliharibu pua yake akiwa mtoto mdogo. Upandikizaji kama huo ulifanywa nchini China mwaka 2013 ambapo mtu mmoja ambaye aliharibu pua yake katika ajali alipewa pua mpya. Wazazi wa Arun walimchukua na kumpeleka katika daktari mwengine katika kijiji cha jimbo la kati la Madhya Pradesh ambapo aliugua kichomi mda mfupi baada ya kuzaliwa. Lakini matibabu aliyopewa yaliongeza hali yake na hivyobasi kupoteza pua yake. Miaka kadhaa baadaye,kundi moja la madaktari katika mji wa Indore liliamua kufanya upasuaji usiokuwa wa kawaida ambapo Arun alipata pua mpya

Leicester yamsajili mshambuliaji wa Nigeria

Klabu ya Leicester City imemsajili mshambuliaji wa Nigeria Ahmed Musa kutoka CSKA Moscow kwa kandarasi ya miaka 4 itakayogharimu pauni milioni 16. Southampton,Everton na West Ham walikuwa wakitafuta saini ya mchezaji huyo. Musa ni mchezaji wa nne kusajiliwa na Leicester baada ya kipa Ron-Robert Zieler ,beki Luis Hernandez na kiungo wa kati Nampalys Mendy. Mchezaji huyo alijiunga na CSKA mwaka 2012 na kufunga mabao 54 kati ya mechi 168 alizocheza,na amefunga mabao 11 katika mechi 58 alizochezea Nigeria tangu aanze kucheza mwaka 2010.

Mamba 100 watoroka hifadhi katika mafuriko

Mamlaka nchini Uchina inajaribu kutafuta takriban mamba 100 waliotoroka kutoka kwenye hifadhi moja baada ya mafuriko makubwa yanayoshuhudiwa nchini humo. Mafuriko hayo yaliwawezesha mamba hao kuogelea na kuondoka kwenye eneo lilizingirwa kwenye hifadhi hiyo katika mkoa wa Anhui. Ni nadra sana kupata Mamba hao wa Uchina mwituni. Hata hivyo mamba huwindwa kutokana na ngozi yao inayouzwa kwa bei ghali mno pamoja na nyama yao na pia hutumika kuwaburudisha watalii. Takriban watu 180 wamekufa maji kutokana na mafuriko hayo makubwa yanayoendelea kushuhudiwa nchini China. Zaidi ya watu milioni moja wamelazimika kutorokea maeneo yenye milima ilikutoroka mafuriko yanayochacha

Mamia kupigwa picha za utupu Uingereza

Mamia ya watu watavua nguo zao na kupigwa picha wakiwa tupu kusherehekea utamaduni katika mji wa Hull, Uingereza. Tukio hilo litakuwa la kusherehekea mji huo kama Mji wa Utamaduni. Washiriki watapakwa rangi ya samawati Jumamosi na kisha wapigwe picha wakiwa katika maeneo mashuhuri jijini humo kama sehemu ya mradi uliopewa jina Sea of Hull. Mradi huo unatekelezwa na mpiga picha Spencer Tunick na unadhaminiwa na taasisi ya Sanaa ya Ferens Art Gallery. Picha zitakazopigwa zitawekwa na kuoneshwa kwa umma wakati wa tamasha ya sanaa ya 2017 itakayoendelea kwa mwaka mmoja. Tunick, anayetoka New York, amewahi kufanya kazi kama hiyo kwingine. Amewahi kupiga picha za watu wengi wakiwa uchi Sydney Opera House, Place des Arts mjini Montreal, Mexico City na mjini Munich nchini Ujerumani Germany. Bw Tunick amesema kazi zake “hugusia historia ndefu ya Sanaa ya utupu”. "Mavazi ni Sanaa ya mtu mwingine,” anasema. “Fashoni ni Sanaa. Kwa kuondoa hilo (mavazi), nitakuwa nafanya kazi...